TAMTHILIA YA KIFO KISIMANI
UTANGULIZI
Tamthilia
ya Kifo Kisimani imeandikwa na kithaka wa Mberia. Toleo la kwanza la
kitabu hiki ililikuwa mwaka wa 2001 na kina chapa nyingi hadi kufikia
mwaka wa 2009.kimechapishwa na Marimba Publications Ltd.
Anwani
Anwani huwa ni jina la kitabu.Mwandishi amefaulu kutumia anwani’Kifo
Kisimani’. Anwani hii inaashiria kifo cha Mwelusi pale kisimani
alipouliwa na Gege.
Pia anwani hii inaashiria kifo cha Wanabutangi baada ya kukosa maji pale
kisimani.Hii ni baada ya kanuni mpya za utekaji maji kutolewa amabazo
ziliwanyima haki za kuteka maji. Maji ni uhai hivyo kupewa siku tatu za
kuteka maji ni kunyimwa uhai yaani kifo.
Jalada
Jalada ni karatasi ngumu inayofunika kitabu ambapo jina la kitabu
huandikwa.Katika tamthilia hii kuna picha ya mtu aliye na huzuni.Mtu
huyu ni kama ako katika shimo. Hii inaashiria shimo la mateso ambalo
Wanabutangi wametiwa na utawala mbaya wa Bokono na vibaraka wake.
Kuna picha inayoashiria machea.Hii inaonyesha matumaini kwa Wanabutangi
baada ya Mwelusi na wenzake kuanza harakati za mabadiliko.Rangi
inayotumika kwa picha ni ya udongo, kuashiria rotuba ya Butangi.
DHAMIRA YA MWANDISHI
Kiini cha jambo au habari iliyoandikwa na mwandishi.Katika Kifo Kisimani
Kithaka wa Mberia ananuia kuamsha au kumchangamsha msomaji kuhusu
utawala mbaya na jinsi ya kuleta mabadiliko na kuuondoa .
Mwandishi anatetea haki za walionyanyaswa.Hivyo lengo kuu la mwandishi
ni kuzindua watu.
PLOTI
Huwa ni mtiririko wa matukio katika kitabu.Tamthilia hii ina onyesho
kumi.Muhtasari wa onyesho hizi ni kama ifuatavyo.
Onyesho la kwanza
Mchezo unaanza asubuhi ambapo viti vimepangwa tayari kwa mkutano wa
Bokono.Mwelusi ambaye ni kijan anaingia uwanjani.Mawazo yake
yanadhihirika kupitia kwa sauti tunayosikia .Yanamkejeli Bokono kwa
ubinafsi wake na kuwanyanyasa wanabutangi.
Kaloo anaingia uwanjani kwa kutayarisha ,anamwona Mwelusi na anadhani ni
mmoja wa waliohudhuria lakini Mwelusi anamwambia alikuwa anapita tu ni
mawazo yaliyomshika mguu.Kaloo anafurahi kwa kuwa Mwelusi anawaza juu ya
Butangi si kama vijana wengine wanavyo waza kuhusu anasa. Mwelusi
anakubaliana naye na kuongeza kuwa ni wakati wa vita. Kaloo hakubaliani
naye na anamuomba amfafanulie matamshi yake. Mwelusi anamwambia kuwa
atamueleza siku nyingine kwa kuwa hahudhurii mkutano na anaondoka.
Mwelusi Batu anaingia kuukagua uwanja, anafurahishwa na viti.Anapoelezwa
kuwa Mbutwe seremala aliyeunda viti anadai kulipwa Batu anasema aje
amwone na amdai malipo ya mbuzi wawili.
Wanawake ndio watakaocheza katika mkutanowa Bokono Mtemi wa Butangi.Batu
anasema kuwa mtemi akifurahi,wanawake watafurahi.Azena anaingia
uwanjani ili kumsaidia kaloo kwa matayarisho.
Batu anaapoondoka Atega anaingia akifuatwa na Mwelusi. Wanashukiwa kuwa
wapenzi kwa kuwa kila mara wanaonekana pamoja.Naye kama Mwelusi,
anawafahamisha hatohudhuria mkutano.Batu anaingia tena uwanjani na
kuamrisha watu waitwe.Gege anaingia uwanjani huku akiwa anapuliza ala ya
muziki. Batu anamwambia ni muziki wa kuvutia, yeye anasema kuwa
anausifia uongozi wa busara wa Butangi. Kaloo anamhakikishai kuwa yeye
na jamaa zake ni wazalendo kamili na hawatasita kuhudhuria mkutano.
Batu anawasaidia kujitayarisha jinsi watamsifia Bokono;Bokono Bokono
milele!!
Baada ya muda kidogo wanagundua kuwa watu hawaji kwa mkutano.Kaloo
anaenda Mingamiwili na kurudi lakini hakuwapata watu huko pia.
Bokono anapofika anapata hakuna watu kwa uwanja anakasirika sana.
Vibaraka wake wanamuahidi kuwa kuna tatizo lakini watalinyoosha. Zigu
anasema kuwa watu wamechochewa na Mwelusi.Hata hivyo Batu anasema kuwa
watamkomesha anayewachochea watu.Baada ya mabo kutulia wote wanaanza
kumsifia Bokono ;Utaongoza Butangi kwa miaka mia moja.
Onyesho la pili
Matukio ni katika makazi ya Mtemi Bokono amabayo ni sehemu ya majengo
ya Utawala wa Butangi.Bokono amesimama huku akiangalia vitu vilivyo
ukutani na mara kwa mara anaguza hiki na kile.mkewe Nyalwe amekaa kitini
raha mustarehe, akjipepea.punde Mgezi anakuja hadi alipo Nyalwe na
kumuambia kuwa chakula kiko tayari.
Wanapokaa kula Bokono hali chakula ana wasiwasi sana. Nyalwe
anapomuuliza ni kwa nini hali anamjibu kwa kejeli na kumuuliza juu ya
vyeo vyake;mke, mwndani na msiri wake.
Nyalwe anamueleza Bokono kuhusu ndoto yake .Bokono anakubali kuwa ana
hofu ya kunyang’anywa utawala.Nyalwe anamuomba abadilishe mienendo yake
na anamuonya dhidi ya vibaraka wake wanoandanganya kuwa anapendwa na
Wanabutangi.
Bokono anapiga nduru kuwa amamwona nyoka ,anasema ameumwa na bafe lakini
wanagundua kuwa hamna nyoka mle ndani ni hofu tu ya Bokono.
Nyalwe anampa Bokono habari kuhusu kijiji cha Mama Agoro ambao
wangependa kuwagawia huzuni.Hii ni baada ya uwanja wao wa watoto
kuchezea umepewa Askari mkuu.Mama Agoro aliahidi kuridi tena na tena
kutetea haki yao.
Onyesho la tatu
Onyeshao hili ni katika gereza. Gereza ni chumba chenye kidirisha
kimoja, kuta na sakafu chafu.
Tunaonyeshwa mateso na dhuluma kwa Mwelusi kutoka kwa Mweke na Talui.
Wanaanza kwa kumita mtukufu mtemi anaponyamaza wanazidi kunchapa na
kumsukuma hapa na pale.
Mwelusi analalamika kuwa taya zake zinawaka moto kwani waliodai wamekuja
kuzungumza naye wanafanya hivyo kwa mateke na makofi.
Wanamhoji Mwelusi na kumuuliza kama yeye ni mwelisi wa Biuki na kama
anatoka kijiji cha Bunyanya na ukoo wa langile.Anapojibu wanamsifu kuwa
yeye ni muungwana na ni kiongozi mzuri sana wa Butangi.
Wanamuuliza kama yeye ndiye kiongozi wa kundi la kabakaba.Wanazidi
kumchapa ili aliri kuwa anahusika na shughuli za ukombozi lakini
Mwelusi anakataa wanazidi kumachapa.
Batu anaingia na kuwakataza kumchapa, anaomba nafasi azungumze na
Mwelusi.
Kwa upole anamshawishi Mwelusi akiri kuwa kiongozi wa wanamapinduzi na
aombe msama kwa Mtemi Bokono.
Mwelusi anapolia juu ya maumivu Batu anamwambia kuwa atapewa dawa nzuri
akitoka gerezani baada ya kuomba msamaha.Batu anamuacha mwelusi peke
yake kwani anadai kuwa akili ya binadamu hufanya kazi vizuri akiwa peke
yake. Anaporudi na kupata welusi hajafanya uamuzi .
Antaka akiri kwamba anatumiwa na majirani ili kuchafua Butangi.
Anapotataa Btu anamwambia kuwa amepotoshwa . Batu anatoa ishara kwa
Askari na kuondoka.
Sura ya nne
Onyesho hili linatokea mbele ya gereza.Andua amemletea ndugu yake
chakula.Askari wanamkataza kumuona na Askari 111 anajaribu
kumdhurumu.Askari wanapanga kula chakula cha mfungwa lakini askari 1
anawakataza na kuwaomba wampe mfunwa chakula chake.anawaambia wenzake
kuwa ni walafi.wanazungumza kuhusu utawala wa mtemi Bokono kama utafikia
kilele au la.
Askari 11 anaeleza jinsi walijaribu kumgeuza mhutumiwa Fulani aache kuwa
jiwe awe binadamu.Walimng’oa kucha za mkono na za miguu, walimgeuza
kuwa popo na baadaye walifika katikati ya miguu yake na kupiga kambi
hapo.badaye walimuua na kumzika msituni.
Onyesho la tano.
Onyesho hili ni nyumbani kwa Tanyauani.Tanya ameketi akidondoa nafaka
katika uteo.Kwenye sehemu nyingine ya ua Gege amekaakaribu na uzio
akiukaguakagua.punde anauachilia na kuanza kujishughulisha na
utengenezaji wa ala ya muziki.
Mamake anamuuliza kwa nini hajaenda kumtizama nduguye, Mwelusi kule
gerezani.Gege anwambia mamayake asimzomee.Anaendelea kutengeneza ala na
kusema kuwa wasichana watamtambua .
Katika kumbukumbu zake Mwelusi anarejea na kumuuliza hali ya uwnaja wa
ngoma. Wazungumza kuhusu hali ya wanabutangi.Gege anamshuritisha
nduguye kwa kujali jamii kila mara na kusahau maisha yake mwenyewe.
Mwelusi anamuomba aieonee huruma Butangi na awe mzalendao.
Andua anarejea nyumbani kutoka kisimani.Anajeraha upande mmoja wa uso
wake.Anamueleza mam yake kuwa hakupigana mbali amechapwa na Askari.
Azena anawatemebelea na kumtuliza Tanay juu ya mwanawe.Anamuomba asife
moyo na azidi kumpelekea chakula.
Onyesho la sita
Onyesho hili ni nje ya gereza pia. Tanya amamletea Mwelusi chakula na
pia anataka kuonana naye.Askari wanchukua chakula na kuahidi kuwa
watampelekea. Tanya anapowaomba Askari kumwona mwanawe Askari 11 na 111
wanamkazata. Askari 1 anamuhurumia Tanya na kuwaomba wenzake wamkubalie
mama huyo kumwona mwanawe.
Baadaye Atega analeta chakula zaidi cha mfungwa pamoja na tembo.Askari
wanakula chakula hiki na Kumuomba askari 1 ampelekee rafiki yake mkate
wa wishwa.
Askari 1 anawahadithia juu ya Makea na ulevi wake.Muda huu wote Mwelusi
amekuwa akikata minyororo kwa tupa.
Baadaye askari 111 napoenda kuchungulia anamwona na kumwita mwenzake
atazame pia.Muda kidogo wanasikia umati wa watu .askari wote wanapotea
Mwelusi anafunguliw gereza na kupotea.
Onyesho la saba
Matukio ya onyesho hili ni katika ukumbi wa utawala wa Butangi.Kuna
mkutano kati ya Bokono na vibaraka wake.Lengo la mkutano huu ni kupata
suluhu la Mwelusi na uchochezi wake.
Kame anasema wamuachilie lakini batu anasema hawawezi kumwachilia
mhuni.Maoni yake ni kuwa Mwelusi anafaa kuuliwa.Batu anasema kuwa
wawandanganye watu kuwa Mwelusi amkufa juu ya ugonjwa wa moyo au
aachiliwe kasha njiani apigwe pembe na nyati.Kame anpinga wazo la
kumwaga damu ya binadamu.
Askari 11 naingia na kuwaarifu kuwa Mwelusi amatoroka gerezani.anapoomba
msamaha Batu anamuonya kuwa lazima wamtafute Mwelusi na waijaribu
kutoroka kutoka Butangi.
Bokono anajiunga nao na anaposikia habari za kutoroka kwa Mwelusi
anakasirika na anawaomba wampe heshima yake. Baadaya anawaomba vibaraka
wake au wazee wamtafute na kumuua.
Batu anatumia Mweke na Talui kumshawishi Gege.Anamwambia amlete pale na
kumshawishi.Mweke na Talui wanafanya walivyo ambiwa na Kumwahidi Gege
ndoa na Alida baada ya kumuua Mwelusi.Wanajifanya wao ni wavuvi wawili
na kuhadithi juu ya ndoa ya Gege na Alida.
Onyesho la nane
Onyesho ni uani kwa Tanya.Tanya anajishughulisha na kazi za
nyumbani.Batu anaingia na kumsalimu.Baada yakuamkiana batu anamwambia
kuwa amakuja kwa ziara ya kirafiki. Sitiari ya kozi na njiwa inatolewa
na Tanya.Batu anaulizia kuhusu Mwelusi .Hii ndio sababu yake kuja kwa
Tanya.
Azena anaingia huku akitembea kwa shida.Anasema jinsi walivyovamiwa na
mali yao yote kuchomwa.Batu anasema kuwa ni majirani wao waliowavamia
lakini azena anasema kuwa ni uongo walivamiwa na wahini wa kulipwa na
kina Batu.
Tanya na Azena wanajikumbusha nyimbo walizomuimbia Bokono.
Mwelusi ana Atega wanatokea na kwa kutumia shingo Tanya anawaelekeza
watoroke.Baada ya Batu kutoweka Mwelusi anaeleza mama yake alivyookolewa
na umati.
Askari wanakuja kwa fujo lakini Mwelusi na Atega wanfaulu kutoroka.
Kame anakuja pia na kufikia sasa Tanya anamkejeli kuwa utawala wa
Butangi umemtembelea imebaki Bokono Mwenyewe.Kame anawaeleza kuwa nyoyo
zao ziko pamoja nay eye ni mmoja wa wanamapindizi.Wote wanaondoka
kuelekea kisima cha mkomani aliko Andua na wanamapinduzi wengine.
Onyesho la tisa
Matukio ya onyesho hili ni kisima cha Mkomani.Ni asubuhi na zigu
amesimama huku macho yake yakilikagua bonde.Kaloo anatokea na anapofika
karibu na zigu zigu anashtuka.zigu anamuulizia kaloo kuhusu maoni ya
wanakijiji wnzake juu ya kannuni mpya zilizotangazwa.Anasema kuwa
kanuni zote za Butangi ni za busara.
Kaloo anamtuma zigu amshukuru Bokono Kaloo anamtuma zigu amshukuruBokono
kwa ajili ya kazi aliyoamuru mototo wake apewe.kaloo hajali juu ya
Butangi yeye anataka awe na uhusiano na Bokono ili apate mali
zaidi.Kaloo anaambiwa kuwa ni vyema aende akamshukuru mwenyewe kwani
hivi karibuni Bokona amekuwa akimtaja mara kwa mara.
Andua anapokuta kuteka maji zigu anamkataza na kumueleza kuhusu
kanuni.baadaye Mwelusi na Atega wanatokea lakini Zigu
hawatambui.Anawazungumzia kuhusu Mwelusi aliye gerezani.Zigu ako tayari
kutetea kanuni za Butangi hata kwa silaha.
Baadaye Gege anakuja na kumdanganya Mwelusi kuwa ametumwa na mama yao
Tanya huku akilia , ni ujumbe muhimu ambazo babayao alimwachia. Wanaenda
chemba na Gege anamuua.Kame anafika amechelewa na wote wankimbia
chemba baada kusikia sauti yenye huzuni.
Onyesho la kumi
Matukio ya onyesho hili ni katika Ukumbi wa Utawala wa Butangi.Kiti cha
mtemi kiko mahali pake,lakini ni kitupu.Batu ymo ukumbini.Punde Mweke
anaingia na baadaye Gege. Wakati Gege anadai malipo yake Baada ya kumuua
Mwelusi ndio anagundua kuwa alidanganywa.Batu anamwahidi kuwa atapata
zawadi ya ardhi.Bokono anapoingia anamwahidi kuwa atapewa jina Mkuki wa
Almasi.
Nyalwe anaingia kwa wasiwasi na kuwaonya kuwa umati wa watu
unakuja.wanampuuza.Hata hivyo wanashangaa kuwa Mweke hajaleta habari
zozote na Zigu pia hakuweko.
Azena anaingia ukumbini kama ameinua panga.Kisha askari1,Kame na
Atega.Atega anamtetea nyalwe asifungwe kwani alikuwa kamwe anatetea
Wanabutangi.Wanawafunga Bokono, Batu,Gege na kuwatoa nje .Watu
wanasherekea ukombozi wao.
WAHUSIKA
Wahusika ni binadamu wa kawaida na wanaendeleza shughuli za kawaida za
kila siku za binadamu.
Mhusika mkuu ni Mwelusi .Ni kiongozi katika shughuli za ukombozi wa
butangi.Anafungwa katika jela na kuteswa sana.(uk 21) onyesho la tatu.
Gege ni nduguye Mwelusi yeye anaendleza maudhui ya ubinafsi.Hana utu,ni
msaliti na pia muuaji kwani alimmuua Mwelusi pale kisimani.
Bokono ni kiongozi mbaya mwenye udikteta.Ananyanyasa na kukandamiza
Wanabutangi.Anawanyima wanabutangi haki zao Kupitia vibara wake Batu na
Zigu.Viongozi hawa ni wakatili,hawana utu. Wanamdanganya Bokono kwamba
anapendwa lakini huo ni unafiki wao.
Tanya na Azena ni wanawake wanao tetea haki za wanabutangi.Tanya ni
Mamake mwelusi na nimkakamavu anazozana na Batu na habadilish msimamo
wake.Uk 76 onyesho la nane.
Atega na Andua ni wasichana ambao wanashiriki katika ukombozi ni
wakamavu, wana ujasiri na pia ni wenye nidhamu hasa Atega kwa kuwapa
askari tembo na kumpelekea Mwelusi tupa.Hawa ni wahusika wasaidizi.
Kuna wahusika wengi kama vile Askari 11 na 111ambao wanaendeleza maudhui
ya ukatili na dhuluma pamoja na Mweke na Talui.
Kame na Askari 1 ni wenye utu na wamezinduka na kushiriki katika
ukombozi.
Kaloo ni kibaraka wa Mtemi Bokono.Yeye hajazinduka.Ni mwenye ubinafsi na
anamtetea mwanawe.Ni mfisadi
MANTHARI
Ni mahali au mazingira yanayotumika katika kitabu. Mazingira ya kawaida
yametumika katika tamthilia hii.Kuna mazingira ya kinyumbani kama vile
Kwa Tanya, Nyumbani kwa Bokono uk 12 onyesho la pili.Kuna mazingira ya
uwanjani, kisimani na gereza.
MBINU ZA UANDISHI NA ZA LUGHA
Kejeli uk 21 Mweke na Talui wanawita Mwelusi Mtukufu Mtemi.Hii ni kejeli
kwani Mwelusi si mtemi mbali ni kiongozi wa ukombozi.Kejeli inasaidia
kuendeleza maudhui ya dhuluma.
Matumizi ya Ndoto uk 14 Nyalwe mkewe Bokono antuhadithia jinsi usiku
mmewe alikuwa akiota na kusema watu wamtoe kaburini. Ndoto hii
inaonyesha hofu ya Bokono kutokana na utawa wake ambao ni mbaya.Ndoto
hii inaendeleza maudhui ya Hofu na utamaushi.
Kuna Nyimbo uk 81Azena na Tanya wanakumbuka nyimbo za kumsifia Bokono.
Wimbo huu unaonyesha Bokono kama kiongozi bora asiye na
kasoro.Wanabutangi waliimuinua Bokono karibu na mungu.Maudhui yake ni ya
uongozi wa kidkteta.
Kuna matumizi ya Taswira.Hizi ni picha zinazojengeka katika akili ya
msomaji.Mwandishi ametumia taswira mbalimbali kama vile gereza.Uk 21
gereza imechorwa kama mahali penye kidirisha kimoja ,kuta na sakafu
chafu. Picha hii inasaidia kuendeleza maudhui ya dhuluma na kunyimwa
haki kwa mfungwa.
Takriri imetumika uk 6 ambapo Kaloo, Azena na Gege wanakariri Bokono
Bokono Milele mara kadhaa.Hii inasaidia kumpa Bokono matumaini ya kuwa
anapendwa.Huu ni Unafiki.Kuna takrir pia katika kurasa zifuatazo uk
8,11,14
Tashhisi imetumika katika ukurasa wa kwanza ambapo sauti inasema kuwa
jua lina bahati,jua lina uwezo uwezo mkubwa. Mwelusi pia anasema mawazo
yamemshika miguu kuonyesha hofu aliyonayo.askari wanasema kuwa siku
inajikokota. Uk 53.Hii inaonyesa ukatili wao na dhuluma na mateso
wanayomletea mwelusi. Andua anaambiwa na Askari asipoondoka
atatemebelewa na makofi.Hii ni dhuluma.
Tashbihi ni ulinganisho wa moja kwa moja wa vitu au watu na wanyama.
Mfano uk71Alida bintiye mtemi ana shingo ya upanga.Hii ni kusaidia
kumshawishi Gege na maelezo haya yanaendeleza unafiki kwani ndoa
anayoahidiwa na hurulaini haipo. Uk 37 Askari wanasema uharibifu wa
mwelusi uko wazi kama meno ya ngiri.
Jazanda ni picha inayomwingia mtu akilini na kuilinganisha na hali ya
kawaida.Mfano uk 61 Batu anaashiriwa kama macho na masikio ya Butangi,
uk64 mwelusi ni mwiba wa Butangi.Hii ni tofauti na jukumu lake la kuleta
mabadiliko katika utawala wa Butangi lakini si kuzuuia maendeleo.
Methali mfano uk55 Batu anasema kuwa dawa ya moto ni moto. Hii ni katika
hatua aliyochukua ya kutumia watu kuvamia kina Azena.Huu ni ukatili wa
kiwango cha juu. Methali pia zimetumika katika kurasa zifuatazo
16,52,39,102 na kadhalika
Chuku ni kutia chumvi au kuongeza sifa ili jambo au kitu kiwe cha
kuvutia. Mfano uk 71 Maelezo ya Alida yametiwa chumvi ili kumvutia Gege.
Katika uk 9 baada ya mambo kutulia na hasira ya mtemi Bokono Kuisha
Batu,Zigu,Kaloo, Azena na wengine waliofika wanaanza kumsifia Bokono
;Utaongoza Butangi kwa miaka mia moja.Hii ni chuku kwani Mtemi
ameshazeeka na hawezi kutawala kwa miaka mia moja.
Chuku pia imetumika katika kurasa zifuatazo 30,72,56 na kadhalika.
Semi uk27 Mwelusi anasema koo lake liko motoni.Hii ni baada ya kichapo
na mateso anayopata gerezani.Semi hii imetumika kuonyesha dhuluma na
mateso kwa Mwelusi. Askari 11 anaeleza jinsi walijaribu kumgeuza
mhutumiwa Fulani aache kuwa jiwe awe binadamu.Walimng’oa kucha za mkono
na za miguu, walimgeuza kuwa popo na baadaye walifika katikati ya miguu
yake na kupiga kambi hapo.Inamaanisha kuwa walimvuta na kumkata na
kumdhulumu sehemu zake za siri.
Semi pia zimetumika katika kurasa zifuatazo 15.27,37 na kadhalika
Mwandishi ametumia Lugha ya Matusi. Hasa katika mazungumzo ya Bokono na
Nyalwe.Mfano mwehu
MAUDHUI
Mambo muhimu yanayoelezwa katika tamthilia.Mwandishi ameshighulikia
maudhu kuu kama vile uongozi mbaya, dhuluma na mateso,ubinafsi na
ukombozi.maudhui mengine ni kama vile usaliti, ubinafsi, utu, unafiki na
uchochezi.
Uongozi Mbaya
Mtemi wa Butangi Bokono pamoja na vibaraka wake Batu na Zigu
wanaendeleza maudhui ya uongozi mbaya. Wanamfanya Mwelusi kukamatwa na
kufungwa gerezani bila makosa yoyote amabayo wanaweza kuthibitisha.
Katika Mkutano batu anaeleza jinsi walichoma kijiji cha Kina Azena na
kusema mfumo wake wa uongoni ni dawa ya moto ni moto.
Kwa kuwa Mwelusi anatetea haki za wanyonge Bokono anamwita mwiba. Hii ni
kwa sababu anazuia yeye na vibaraka wake kujichumia mali. Mwishowe
wanamtumia Gege kumuua.
Wanaamua kuwanyima Wanabutangi haki ya kuteka maji pale kisimani. Mtemi
anauliza kamawamewatangazia watu kuhusu kanuni mpya ya kuteka maji
kisima cha Mkuyuni kuwa ni siku tatu kwa wiki.
Dhuluma Na Mateso
Askari 11 anaeleza jinsi walijaribu kumgeuza mhutumiwa Fulani aache
kuwa jiwe awe binadamu.Walimng’oa kucha za mkono na za miguu, walimgeuza
kuwa popo na baadaye walifika katikati ya miguu yake na kupiga kambi
hapo.badaye walimuua na kumzika msituni.uk 43
Mwelusi anafungwa gerezani kama hakuna kesi na hajahukumiwa.Batu
anapomtemebela baada ya kumshawishi akiri kutochochea Wanabutangi na
kushindwa anawaagiza Askari wazidi kumchapa na kumtesa.uk 29
Katika uk 30 Mwelusi anasema anachomwa na mikuki mia moja na anaelezwa
kama anayeumia.Hii ni kutokana na kichapo anachopata kutoka kwa Askari.
Uk49 Andua anasema kuwa hakupigana alipigwa na ndia sababu ako na jeraha
upande mmoja wa uso wake.Anasema kuwa ni Ni Askari waliwapiga kule
kisima cha Mkuyuni baada ya wao kwenda kuteka maji.
Askari wa Butangi kulingana na Tanya si wa kulinda mbali ni wa kuleta
mateso na kuwachapa Wana butnagi. Tanya anasema kuwa juzi walimngoa
motto wa Chendeke meno.
Uk 24 Mweke na Talui wanapokuja kuzungumza na Mwelusi wanafanya hivyo
kwa makofi na mateka.Mwelusi anasema kuwa taya zake zinawaka moto.
Batu anajaribu kuukinga uongozi wa Bokono na amamuomba mwelusi kuacha
uchochezi na kuomba msamaha.Mwelusi anapokataa kukiri kwamba anatumiwa
na majirani ili kuchafua Butangi. Anapotataa Batu anamwambia kuwa
amepotoshwa . Batu anatoa ishara kwa Askari na kuondoka. Yeye anawpa
ruhusa Askari wamtese mwelusi badala ya kumlinda.uk 36
Ubinafsi
Tunauona ubinafsi wa Gege .Uk wa 95 Gege anamuua Mwelusi nduguye ili
apate kuozwa Alida bintiye Mtemi. Uk 17 anamuambia Mwelusi ajali maisha
yake aachane na jamii. Gege hajali maisha ya wnabutangi wengine
anajijali yeye mwenyewe.
Uk 89 Kaloo anamtuma zigu kwa Bokono amshukuru kwa ajili ya kazi
aliyoamuru mototo wake apewe.kaloo pia hajali juu ya Butangi yeye
anataka awe na uhusiano na Bokono ili apate mali zaidi.
Gege hajaenda kumtizama nduguye, Mwelusi kule gerezani.Gege anwambia
mamayake asimzomee anapoulizwa.Anaendelea kutengeneza ala na kusema kuwa
wasichana watamtambua .Hivyo anajali sana wasichana kuliko nduguye.uk43
Ukombozi
Mwelusi,Atega.Andua,Kame na Askari 1 ni baadhi ya wanamapinduzi katka
Butangi.
Watu hawa wanapinga utawala wa Mtemi Bokono na vibaraka wake.
Wakati Mwelusi amefungwa gerezani Atega anamletea mkate wa wishwa ukiwa
na tupa ambayo anatumia kukata minyororo na kujikomboa. Baadaye umati wa
watu wanakuja na kumsaidia kufungua gereza na kujikomboa.uk 59
Kwa Uongozi wa Mwelusi wanaendelea kutetea haki zao.Mfano Andua anaenda
kisimani kuteka maji.
Hata baada ya mwelusi kuuliwa na Gege wanamapinduzi hawa wanaendelea na
harakati zao za ukombozi. Uk 105
Kitabu kinaisha kama Bokono,Batu,Zigu , Mweke na Gege wamefungwa kamba
baada ya kufumaniwa na Waandamanaji.Hivyo wanaukombozi wanafaulu
kukomboa Butangi kutokana na utawala Mbaya.
Mwelusi anadaiwa kuwa yeye ndiye kiongozi wa kundi la kabakaba.
Anahusika na shughuli za ukombozi.Ni yeye kiongozi wa kundi hili la
wanamapinduzi.
Usaliti
Gege anamsaliti kakake, Mwelusi kwa Kumuua pale Kisimani. Uk 95 Gege
anamdanganya Mwelusi kuwa ametumwa na mama yao Tanya huku akilia , ni
ujumbe muhimu ambazo babayao alimwachia. Wanaenda chemba na Gege
anamuua.
Viongozi wa Butangi ikiwemo Batu na Zigu wanawasaliti kwa kuwanyima haki
zao na kuwatesa.
Utu
Kame Askari 1 ni wenye utu wanamtetea Mwelusi.
Uk 60 wakati Batu na zigu wanataka kumuua Mwelusi Kama anasema
wamuachiliea kwa kuwa hana makosa yoyote.
Uk 35 Tanya anapowaomba Askari kumwona mwanawe Askari 11 na 111
wanamkazata. Askari 1 anamuhurumia Tanya na kuwaomba wenzake wamkubalie
mama huyo kumwona mwanawe.
Hawa wawili paoja na wengine kama vile Azena na Atega ni wenye utu
miongoni mwa wanabutangi wengi ambao wana unyama kama vile Batu.
Askari wanapanga kula chakula cha mfungwa lakini Askari 1 anawakataza na
kuwaomba wampe mfunwa chakula chake.uk 37
Unafiki
Uk 25 Mweke na Talui wanamhadithia Gege jinsi harusi yake na Alida
itakavyokuwa. Wanamwambia Gege amuue Nduguye Mwelusi na atapewa mali
pamoja na kuoa mtotot wa Mtemi Bokono.
Wakati Gege anaenda kudai malipo yake Baada ya kumuua Mwelusi ndio
anagundua kuwa alidanganywa.Talui na Mweke ni wanafiki walijua kuwa
wanamdanganya Gege ili awasidie tu kumumaliza Mwelusi.
Batu anapomtemebelea Mwelusi gerezani anamwambi a kuwa ni rafiki yake na
kumuomba ajiunge naye katika kuitumikia Butnangi.Huu ni unafiki kwani
kabla ya hapo alipokuwa kwenye mkutano na Zigu na Kame alpanga jinsi
watakavyo muua.
Uk 79 Batu anapomtembelea Tanya anamwita rafiki yake tangu ujana
wao.huu ni unafiki kwani Batu yuko pale kumtafuta Mwelusi.
Baada ya kumuahidi Tanya kuwa watampa Mwelusi chakula Askari wanakula
chakula hiki na Kumuomba askari 1 ampelekee rafiki yake mkate wa wishwa.
Uk 58. Huu ni unafiki.
Uchochezi
Kabla mkutano uanze Mwelusi anafika pale na kudai kuwa anapita.Hata
hivyo nia yake wakiwa na Atega ni kuwachochea watu wasuhudhurie mkutano
wa Mtemi Bokono.Uk 1
Uk wa 9 Zigu anasema kuwa kuna fununu ya kuwa kuna kijana anayechochea
watu.Kijana huyu ni Mwelusi.
Uk 90 Zigu anamwambia Kaloo kwamba Bokono amekuwa akimtaja mara kwa
mara.Zigu ananchochea Kaloo aonane na Bokono na kumpa shukrani yeye
mwenye kwa kazi ambayo Bokono alamuru motto wa Kaloo apewe.
FALSAFA YA MWANDISHI
Mwandishi analenga kuzindua wananchi kuhusu utawala mbaya.Anatetea haki
za walionyanyaswa na kukandamizwa. Anashikila kuwa kuna uwezo wa
kujikomboa kutoka kwa uongozi mbaya .Hii ni kupitia kwa watu kuungana na
kuandama na kutetea haki zao na kubadilisha uongozi mbaya ,pamoja na
kuwafungaviongozi wabaya.
Falsafa ya Kithaka ni haki na hukumu kwa wenye makosa.
NADHARIA
Mwandishi ametumia Nadharia kama vile Umaksi.Katika Butangi wenye mali
wananyanyasa wasio na mali.Kuna Ufeministi kwani Atega ,Andua Tanya na
Azena ni wahusika wa kike wanaoshiriki katika ukombozi.Kuna Uhalisia
Kwani matukio ni ya kawaida kam vile uongozi mbaya na kunyimwa haki
katika maisha ya kila siku. Kuna Utamaushi kwani wanabutangi wamekata
tama.Mfano Tanya anamtaka Mwelusi aondoke Butangi
HITIMISHO
Mwandishi amefaulu kutumia mbinu na kutoa maudhui kwa kutumia nadharia.
Kithaka anatetea haki kwa wenye Kunyanyaswa na hukumu kwa wenye
makosa.Amewatumia wahusika wa kawaida kuutoa ujumbe wake.
Kuna udhaifu katika anwani kwani sio wahusika wote wanaathiriwa na kifo
kisimani.Kitabu kimeshughulikia zaidi ya kifo.
UHUSIANO KATI YA TAMTHILIA YA KIFO KISIMANI NA UTENZI W A FUMO LIYONGO
Utenzi wa fumo liyongo unamhusu shujaa Liyongo kutoka jamii ya
waswahili.liyongo alishuhudiwa na jamii yake na makabila jirani kama
vile wagalla.
Hata hivyo mfalme wa pate(Daudi Mringwari) alimchukia kwa kuhofu kuwa
angemnyang’anya utawa wake.Hivyo alipanga njama za kumwangamiza
liyong.Akamtia gerezani alikolindwa na Askari wake.Akiwa gerezani,
aliletewa mkate wa wishwa uliotiwa tupa.Aliitumia tupa hii kukata
minyororo kasha akotoroka.
Mfalme wa pate hakukata tama.Alimshawishi mwanawe Liyongo kumuua babake
na kumwahidi kumwoza bintiye.Liyongo akauliwa na mwanawe kwa kumfuma
msumari wa shaba kitovuni.Liyongo alifia kisimani na kuwatisha watu
wasichote maji kwa siku kadhaa.
Utenzi huu kwa kiasi kikubwa unahusiana na tamthilia ya Kifo Kisimani,
inayomhusu Mwelusi anayepinga utawala dhalimu wa Mtemi Bokono.
Anachukiwa na Bokono pamoja na vibaraka wake kwa hofu kuwa atauangusha
utawala huo.Anatiwa gerezani lakini anatoroka baada ya kukata minyororo
kwa tupa iliyotiwa ndani ya mkate wa wishwa alioletewa na Atega. Bokono
anamtumia nduguye Mwelusi, Gege kumuua kwa kumdunga kisu pale kisimani.
Gege vilevile anaahidiwa na Mweke wakiwa na Talui kuwa ataozwa bintiye
mtemi.Alida.
Hata hivyo kuna tofauti nyingi kati ya tungo hizi mbili. Fumo Liyongo ni
mhusika wa kihistoria, aliishi baina ya karne 15 na 16.Mwelusi naye ni
mhusika wa kubuni.Fumo alikuwa na sifa za kiajabu kama vile nguvu
zilizokithiri, mpiganaji hodari aliyeshinda vita vingi, ukubwa uliopita
kiasi na uwezo wa kutambua mabo kabla hayajiri.Mwelusi hana sifa kaa
hizi zinazomtambuliasha kama mhusika wa kipekee.Vita anavyopigana si vya
silaha bali anapinga dhuluma na mateso kwa Wanabutangi.
MAREJELEO.
1. Kithaka wa Mberia, (2001) Kifo Kisimani, Marimba Publications
limited, Nairobi Kenya.
2. Rocha M.Chimera, (1998) Kiswahili; Past, Present and Future
Horizons,Nairobi University Press,.Nairobi.
UKUMBI WA LUGHA
Sunday, 29 January 2017
Friday, 29 July 2016
sajili katika lugha
Sajili
Ni matumizi ya lugha katika muktadha mbalimbali.Kuna sajili anuwai za matumizi ya lugha katika jamii. Hapa tutazingatia mifano michache ya sajili mbali mbali.Kila sajili huwa na sifa mbalimbali zinazoitofautisha sajili hiyo na nyinginezo. Ili kubaini sifa za lugha katika sajili fulani, ni muhimu kuzingatia baadhi ya maswali yafuatayo:
· ni mazungumzo baina ya nani na nani?
· kuna uhusiano gani baina ya wanaozungumza?
· yanapatikana wapi?
· yanatumika katika hali gani?
· yana umuhimu ama lengo gani
· ni istilahi zipi istilahi (maneno maalum) zinazopatikana katika mazingira hayo?
· umaizi wa lugha baina ya wazungumzaji ni wa kiwango gani?
· ni mtindo gani wa lugha unaotumika?
Sajili ya Ajali
Hii ni lugha inayotumiwa katika ambalo ajali imetokea. Wahusika wanaweza kuwa majeruhi, polisi, walioshuhudia au wananchi wengine n.k
Sifa za lugha inayopatikana katika sajili hii
1. Msamiati wa kipekee unaohusiana na ajali kama vile majeruhi, hudumanya kwanza, damu, mkasa.
2. Hutumia lugha ya kudadisi dadisi ili kubaini chanzo cha ajali.
3. Huwa na masimulizi – walio na habari kuhusu kisa hicho hueleza waliyoshuhudia
4. Kutokana na hali ya msukosuko, lugha hii haina utaratibu – watu huwa katika hali ya hofu, kwa juhudi za kuwaokoa majeruhi.
Mfano wa Sajili ya Ajali
Mwanakijiji 1:
Nimesikia twa! Kisha kishindo kikubwa sana (akihema hema) Nikaambia kuna mlipuko tukimbie.
Mwanakijiji 2:
Lilio la muhimu ni kuyaokoa maisha ya majeruhi kwa kuwapa huduma ya kwanza.
Mwanakijiji 1:
Tuondoeni miili ya waliofariki kwanza.
Mwanakijiji 2:
hatuwezi kuishika miili iliyobanwa katika gari hadi polisi wafike. Na ndio hao wanaokuja!
Mwanakijiji 1:
(akikimbia) Ndio hao! Acheni kuiba mafuta! Polisi wanakuja!
Polisi:
Wakitawanya wananchi walioliparamia gari kuiba bidhaa mbali mbali.Liinueni hili gari! Wapi dereva?
Dereva:
(ambaye amelala akihema kwa maumivu, damu ikichuruzika miguuni na mikononi) Nilisitishwa na ng'ombe waliokuwa wakivuka barabara. Nilijsribu kukwepa lakini usukani ukanishinda gari likapoteza mwelekeo…
Abiria:
Alikuwa akiendesha gari kwa kasi sana. Tukampigia kelele apunguze mwendo lakini hakutusikia. Matunda yake…
Mwanakijiji 2:
Niliona gari likibingiria mara kadhaa mpaka likaingia humu mtaroni, ndiyo tukakimbia kuwaokoa.
Polisi:
Nyamazeni! Achieni polisi kazi iliyobaki. Ikiwa kuna yeyote anayejuana na waathiriwa aandamane nasi.
Sajili ya Biashara
Lugha ya biashara huzungumzwa na wauzaji na wanunuzi katika sehemu za kibiashara. Inapaswa ikumbukwe kwamba lugha hii inaweza kubadilika kidogo kulingana na mazingira. Kwa mfano, katika mikutano ya kibiashara, lugha rasmi hutumiwa ilihali katika soko, lugha ya mitaani inaweza kutumika.
Sifa za Lugha ya Biashara
1. Hutumia msamiati wa kibiashara kama vile:
· Fedha
· Faida
· Hasara
· Bei
· Bidhaa
2. Hutumia misimu ili kuwavutia wanunuzi
3. Ni lugha yenye malumbano hasa watu wanapojadiliana kuhusu bei
4. Ni lugha legevu - haizingatii kanuni za lugha.
5. Huchanganya ndimi kwa kuingiza maneno ya lugha za kigeni
6. Ni yenye heshima na unyenyekevu kwa wanunuaji
7. Msamiati katika lugha ya Kibiashara
Mfano wa Sajili ya Biashara
Mtu X:
Tatu kwa mia! Tatu kwa mia! Leo ni bei ya hasara!
Mtu Y:
Unauza hii briefcase kwa pesa ngapi?
Mtu X:
Hiyo ni seventy bob mtu wangu
Mtu Y:
Huwezi kunipunguzia. Niuzie hamsini hivi.
Mtu X:
Haiwezekani mtu wangu. NItapata hasara nikiuza hivyo. Ongeza mkwaja, mama.
Mtu Y:
Basi hamsini na tano.
Mtu X:
Tafadhali ongeza kitu kidogo. Unataka nikule hasara leo? Fikisha sitini na tano.
Mtu Y:
Basi sitanunua hii. Sina pesa hizo zote. Unajua uchumi ni mbaya siku hizi.
Mtu X:
Tafadhali mtu wangu. Huu mkoba ni mzuri sana. Umetoka Germany. Angalia. Unaweka pesa hapa, kitambulisho hapa halafu unafunga hivi. Hauwezi kupoteza chochote ukiwa na mkoba huu. Angalia wewe mwenyewe. Hakuna mahali pengine utaweza kununua mkoba huu kwa bei ghali kama hii.
Mtu Y:
Nimekwambia sina hizo pesa. Nitanunua baadaye ukipunguza bei.
Mtu X:
Lete sixty bob. Lakini utakuwa umeniumiza. Nakufanyia hivyo kwa kuwa wewe ni customer poa.
Mtu Y:
Sawa basi nitanunua. Shika sixty bob.
Mtu X:
Asante Customer. Mungu akubariki. (akimfungia) Hey! Tatu kwa mia. Bei ya hasara! Tatu kwa mia!
Sajili ya Bungeni
Hii ni lugha inayozungumzwa wakati wa kikao cha bunge. Sajili hii ni tofauti na na sajili ya siasa, ambayo huhusisha wanasiasa wakipiga kampeni.
Sifa za Lugha ya Bungeni
1. Ni lugha yenye ushawishi – wabunge hutumia vishawishi ili kuwahimiza wenzao waunge ama kupinga msalaba
2. Ni lugha ya mjadala yenye waungao na wapingao.
3. Ni lugha yenye heshima na nidhamu. Maneno ya heshima kama mheshimiwa, tafadhali na samahani hutumika sana.
4. Hutumia maneno maalum yanayopatikana katika mazingira ya bunge kama vile kikao, mswaada, kuunga mkono, kujadili, kupitisha, n.k.
5. Lugha ya bungeni ni rasmi na sanifu.
6. Hulenga maswala mbalimbali ya kisiasa na maendeleo katika taifa.
7. Huwa na maelezo kamilifu
8. Ni lugha yenye maswali na majibu miongoni mwa wabunge.
Mfano wa sajili ya Bungeni
Spika:
Waheshimiwa, muda unayoyoma. Nawaomba mfanye mazungumzo yenu sauti ya chini tumsikize huyu. Endelea mheshimiwa.
Mbunge 1:
Asante Bwana spika. Hii siyo mara ya kwanza ya kuuwasilisha mswaada huu hapa. Kila mbunge anayethamini raia wa taifa hili ni lazima auunge mkono mswada huu. Katika kikao kilichotangulia, mliupinga mkidai kwamba hauna heshima kwa rais. Leo tumefanya ukarabati wote mliotaka. Hamna budi kuuunga mkono. Bwana spika….
Spika:
Muda wako umekwisha tafadhali keti. Wabunge wataamua hatima ya mswada huu ikiwa utapitishwa kama sheria. Lakini kumbukeni uamuzi wa mwisho ni wa rais
Sajili ya Hospitalini
Hii ni lugha ambayo huzungumzwa katika hospitali baina ya madaktari, wagonjwa, wauguzi n.k
Sifa za Lugha ya Hospitalini
1. Hutumia msamiati wa hospitalini kama vile
· dawa
· magonjwa
· Daktari
· Wadi
· Mgonjwa
· Dawa
· Kipimo
2. Ni lugha yenye upole na heshima
3. Huwa na maswali mengi hasa daktari anapotaka kutambua kiini cha ugonjwa unaomhadhiri mgonjwa wake
4. Ni lugha yenye hofu na huzuni
Mfano wa Sajili ya Hospitalini
Daktari:
Ulianza kuumwa hivi lini?
Mgonjwa:
Kichwa kilianza kuniuma jana jioni baada ya chajio. Nilipoamka asubuhi nikatambua kwamba hata tumbo lilikuwa likiuma pia.
Daktari:
Ulipoanza kuumwa na mwili mzima, ulichukua hatua gani? Hukunywa dawa yoyote?
Mgonjwa:
Nilichukua tembe zilizokuwa zimepatiwa kakangu miaka mitano iliyopita alipokuwa akiumwa na malaria.
Daktari:
Kila ugonjwa huitaji matibabu mbalimbali. Tembe za malaria haziwezi kutumika kutibu maumivu ya kichwa na tumbo. Pia ni hatari kutumia dawa ambazo zimepitwa na wakati. Zinaweza kukuletea madhara zaidi.
Mgonjwa:
(akikohoa) Sijui kama una tembe za kifua pia. Hii baridi inaniletea homa mbaya.
Daktari:
Hatuwezi kukupatia dawa kabla ya kutambua ugonjwa ulio nao. Itabidi tupime joto lako, damu na pia mate yako ili kupata tatizo linalokusumbua. Kisha tutakupatia dawa. Je, una umri wa miaka mingapi?
Mgonjwa:
Nikichukua hizo dawa nitapona?
Daktari:
Matokeo hubadilika kutoka kwa mgonjwa mmoja hadi mwengine. Inaweza kuchukua muda. Huenda ukalazwa kwenye wadi kwa siku mbili tatu hivi. Umri wako, mama?
Sajili ya Kidini
Katika sajili ya kidini tunaangazia lugha inayozungumzwa na waumini/washiriki wa imani fulani wakati wa ibada, sala, katika nyumba takatifu au mahali popote pale ambapo wanazungumzia mambo yanayorejelea imani au Mwenyezi Mungu.
Sifa za Lugha ya Kidini
1. Hutumia msamiati wa kidini kama vile
· Bibilia
· maombi
· mbinguni
· jehanamu
· Madhabahu
· Paradiso
· Mbinguni
· Mwenyezi Mungu
· Mwokozi
2. Ni lugha inayonukuu sana hasa wazungumzaji wanaporejelea Kitabu kitakatifu
3. Lugha yenye heshima, upole na unyenyekevu
4. Lugha sanifu
5. Ni lugha iliyojaa ahadi nyingi kwa wanaoandamana na mafunzo ya kidini na vitisho kwa wanaoenda kinyume na mafundisho
6. Huwa imejaa matumaini
7. Ni lugha yenye kutoa maneno ya sifa, kumtukuza na kumshukuru Mwenyezi Mungu
Mfano wa Sajili ya Kidini
Boriti:
Bwana asifiwe Bi...
Bi Rangile:
Amina, mchungaji. Watoto wanaendeleaje?
Boriti:
Karita hana neno. Mwenyezi Mungu ametunyeshea rehema na neema zake. Je, wajukuu wako wa hali gani?
Bi Rangile:
Wanaendelea vizuri isipokuwa hawataendelea na masomo. Sijui nilimfanyia Mungu dhambi gani.
Boriti:
Nasikitika sana kusikia hivyo. Mungu atawalinda mayatima hao. Yeye ndiye baba wa mayatima. Mungu ni mwenye huruma.
Bi Rangile:
Sijui hayo, mchungaji. Hata sijui maana ya kuishi hapa duniani. Kila siku ni matatizo.
Boriti:
Usife moyo. Mungu anasema katika kitabu cha Yohana 14:18, "Sitawaacha nyinyi kama mayatima..." Kwa hivyo, ukiwa na imani, Mungu atakuonekania.
Bi Rangile:
Basi niombee mchungaji ili Saumu na Neema wapate karo ya kurudi shuleni.
Boriti:
Funga macho tusali. Ewe Rabuka uliyejaa neema na baraka tele. Tunakushukuru na kulitukuza Jina lako takatifu kwa baraka zako za ajabu. Tunajua kwamba wewe ndiye Mungu uliyewatoa wana wa Israeli kutoka Misri. Sisi wenye dhambi tunakuja mbele yako tukiomba ukafanya miujiza katika nyumba hii ya Bi Rangile......
Wote:
Amina.
Sajili ya Kisayansi
Sifa za Lugha katika sajili hii
1. Hutumia msamiati wa kipekee unaoambatana na taaluma inayorejelewa.
2. Huwa na maelezo kwa ukamilifu.
3. Huwa na mpangilio maalum na maendelezo ya hoja na ujumbe.
4. Huchanganya ndimi na kutumia maneno ya kisayansi au lugha mbalimbali.
5. Hutumia lugha sanifu.
6. Ni lugha yenye udadisi mwingi (wakati wa kufanya utafiti)
Kwa sababu zisizoweza kuepukika, kikundi chetu hakitamaliza utafiti ulioratibiwa kukamilishwa mwishoni mwa mwezi ujao. Hii ni kwa sababu ya changamoto kadhaa ambazo tumekutana nazo. Kwanza, viluwiluwi, ambao ndio tunaotafiti wamekuwa haba sana wakati huu wa ukame. Pili, kutokana na kufungwa kwa maabara ya kisayansi katika taasisi hii, ni muhali kufanya majaribio yoyote ya kazi yetu. Tatu, kumekuwa na pingamizi kubwa kutoka kwa baadhi ya wanakijiji kwamba kukusanya viluwiluwi kunawatia hofu. Aidha, tume yetu imepungukiwa na fedha baada ya serikali kusitisha kudhamini utafiti huu.
Baada ya kujadiliana kwa vikao tatu mfululizo, tume yetu inapendekeza haya: Muda wa kufanya utafiti uongezewe kwa kipindi cha miezi sita; serikali kupitia kwa taasisi hii ifadhili wachunguzi. Wananchi wahamasishwe kuhusu umuhimu wa kuwafanyia viwavi utafiti na maabara ya utafiti ikaraatiwe haraka iwezekanayo.
Sajili ya Mahakamani
Hii ni lugha inayozungumzwa na wanasheria, mahakimu, mawakili, washitakiwa na mashahidi katika mahakama.
Sifa za Lugha ya Mahakamani
1. Hutumia msamiati wa kipekee unaorejelea sheria kama vile
· katiba
· sheria
· mashtaka
· Hakimu
· Ushahidi
· Wakili
· Jela
· Mshitakiwa
· Kiongozi wa mashtakiwa
2. Huwa na maelezo marefu na ya kina ili kutafuta ushahidi wowote uliopo
3. Ni lugha yenye kunukuu sana hasa vipengele katika vitabu vya sheria kama vile katiba
4. Ni lugha rasmi na sanifu
5. Ni lugha iliyojaa maswali na majibizano
6. Ni lugha yenye heshima
Mfano wa Sajili ya Mahakamani
Kiongozi:
Musa Kasorogani, mwanaye Bi Safina na Mzee Mpotevu Kasorogani; umeshtakiwa kwa kosa la jaribio la mauaji mnamo tarehe 23/08 mwaka huu. Unaweza kukubali mashitaka, kukana au kunyamaza. Je, unakubali mashitaka.
Musa:
Naomba kukanusha mashtaka hayo, bwana mkubwa.
Kiongozi:
Je, kuna shahidi yeyote katika kesi hii?
Katili:
Hapa mkubwa. Siku hiyo ya tarehe 23/08, Musa alipatikana akiwa akijinyonga usiku wa maneno. Kijiji chote kilikusanyika hapo kwenye boma ya Kasorogani. Nilipoleta polisi, wakamkamata na kumpeleka hospitalini atibiwe kwanza. Ndiposa ameletwa hapa siku ya leo.
Kiongozi:
Je, mshitakiwa una tetesi lolote. Ama pia unaweza kuleta wakili wako azungumze kwa niaba yako.
Kisaka:
Bwana mkubwa, mimi ndiye wakili na shahidi wa Musa. Musa hakuua mtu. Alikuwa akijinyonga kutokana na mkasa uliomfika tarehe hiyo ya Agosti 23 baada ya bibi harusi wake kubadilika. Mimi na mamake, Bi Safina Kasorogani tulijaribu kumtuliza jioni hiyo. Asubuhi nilipoamka siku iliyofuatia, nikapata habari kwamba alikuwa amepelekwa hospitalini. Je, alipojaribu kujiua, alimwua mtu yeyote?
Kiongozi:
Kulingana na katiba ya nchi hii, kifungu cha 12.ab, kuua ni kutoa uhai wa binadamu yeyote. Haijalishi ikiwa ni yeye mwenyewe au ikiwa ni rafiki yake. Hivyo basi jaribio la kujiua ni hatia kulingana na kanuni za nchi hii. Una jingine la kuulizia?
Kisaka:
Je, sheria yetu inaruhusu mtu kuadhibiwa kwa kosa ambalo hakufanya?
Kiongozi:
La hasha.
Kisaka:
Basi tutakuwa tumekiuka kanuni za nchi yetu iwapo tutamhukumu Musa kwa kujiua ilhali hakujiua bado. Tunawezaje kutambua kama angekufa?
Katili:
Inafaa ahukumiwe kinyonga au kifungo cha maisha gerezani. Hata alivunja simu yangu...
Kiongozi:
Order! Lazima kutii mpangilio wa mahakama. Katili hauruhusiwi kuongea bila ruhusa ya hakimu au kiongozi wa mashitaka. Polisi, mpelekeni nje.
Sajili ya Matanga
Ni lugha inayotumiwa katika shughuli za mazishi au nyumbani kwa marehemu.
Sifa za Lugha ya Matanga/Mazishi
1. Hutumia msamiati wa maneno ya huzuni kama vile waombolezaji, makiwa, kifo, mauti, pole n.k.
2. Hutumia lugha ya kuliwaza/kufariji na kupa matumaini hasa kwa waombolezaji.
3. Ni lugha yenye unyenyekevu isiyotumia maneno yanayokera.
4. Hudhihirisha unyonge wa mwanadamu, kama asiye na mamlaka juu ya uhai wake.
5. Huwa na mbinu rejeshi kurejelea maisha ya marehemu alipokuwa hai.
6. Kwa mara nyingi hutumia maneno ya kusifu marehemu kutokana na aliyotenda.
7. Wakati mwingine huwa ni lugha inayodhihiri hali ya kukata tamaa.
Mfano wa Sajili ya Matangani
"Waombolezaji wenzangu, kama mnavyojua tumekusanyika hapa kwa ajili ya kumsindikiza rafiki yetu amabye amelala hapa. Ikiwa kuna mtu alifikwa zaidi na msiba huu ni mimi. Marehemu alikuwa rafiki wangu wa dhati tuliyeshirikiana naye sana. Nilimjua marehemu tukifanya kazi katika soko la Mauzoduni na tangu siku hiyo tumeishi kama ndugu; kuomba radhi ukikosewa; kusaidiana, na kadhalika.
Habari za kifo chake zilinipiga kwa mughdha. Sikuamini kwamba amekufa; kwamba sitamwona tena aushini mwangu. Ninasikitika sana lakini kwa kuwa Mungu hakosi, ninaamini kwamba alimpenda zaidi ya tulivyompenda. Ombi langu kwa Mungu ni moja, kwamba amweke rafiki yangu mahali pema peponi; au popote alipojitafutia siku zake za uhai; nami nitakapokufa anipeleke papo hapo tuendelee kuwa marafiki. Mwenzangu lala. Lala salama tutaonana siku moja"
Sajili ya Michezoni
Lugha ya michezoni hutumiwa wakati wa mashindano ya michezo kama vile kandanda, ukimbiaji n.k Hii inaweza kuwa lugha ya watangazaji/wasimulizi wa mchezo, watazamaji, mashabiki au wachezaji.
Sifa za Lugha ya Michezoni
1. Hutumia msamiati wa kipekee unaohusu michezo kama vile mpira, goli, mchezaji
2. Huchanganya ndimi na kuingiza maneno ya lugha nyingine kama vile Kiingereza. mfano 'goal!!!'
3. Ni lugha ambayo hutumia vihisishi na mshangao kwa wingi
4. Sentensi nyingi katika lugha hii huachwa bila kukamilika hasa hali inapobadilika uwanjani
5. Husimuliwa kwa haraka haraka ili kuambatana na kasi ya mchezo
6. Ni lugha yenye sifa na na chuku kwa mfano msimulizi anaposimulia sifa za mchezaji fulani
7. Hutumia misimu kama vile 'wametoka sare'
8. Hutumia kwa ya kulinganisha ili kuelezea matokeo ya mechi k.m 'walitoka mbili kwa nunge'
9. Ni lugha yenye kukariri (kurudia rudia) hasa mchezaji anapoumiliki mpira kwa muda mrefu au mwanariadha fulani anapoelekea kushinda katika mbio.
10. Huwa na sentensi fupi fupi
Mfano wa Sajili ya Michezoni
Nakwambia ndugu msikilizaji hapa mambo yamechacha kwelikweli. Hawa wachezaji wa Manyuu hawacheki na watu leo. Wameamua kuishambulia timu ya Cheusi bila huruma. Kumbuka kwamba hii ni mara yao ya... Lo! Anauchukua mpira pale, mchezaji nambari tisa... Matiksta. Matiksta, Matiksta na mpira. Anaucharazacharaza pale. Anamwangalia mwenzake. Anaupiga mpira kwa kichwa pale! Lo! Mwenzake anaukosa. Akiushika mpira pale ni mchezaji wa timu ya Cheusi, Romana. Romana, Romana anaelekeza mpira kwenye lango la Manyuu. Anaupiga mpira kwa nguvu! Lo! Hatari sana. Hatari sana katika lango la Manyuu. Hatari! hatari! Goooooooooo ooooh! Wameukosa! Goal keeper ameudaka mpira huo. Pole sana wachezaji wa ... Mlinda lango anaupiga mpira huo kwa hasira. Juu kabisa. Anauchukua pale nambari saba, Saruta. Huyu ni mchezaji machahari sana. Mwaka uliopita, alipewa tuzo la mchezaji bora wa mwaka. Ananyang'anywa na mchezaji mwingine hapa. Wanakabiliana kidogo. Huyu mchezaji anaupiga mpira kwa mguu wa kushoto. Lo! Mpira umekuwa mwingi na ukatoka nje.
Mashabiki wa timu hizi mbili wanasubiri kwa hamu na ghamu kutambua ni nani atakayeibuka mshindi. Katika mechi zilizotangulia, timu hizi zimekuwa zikitoka sare. Lakini leo lazima mshindi atapatikana. Hawa ni fahali wawili. Kumbuka kwamba unapata matangazo haya moja kwa moja kupitia idhaa yako uipendayo, redio nambari moja kote nchini... Mpira unarudishwa uwanjani. Akienda kuurusha pale ni...
Sajili ya Mitaani
Lugha ya mitaani ni lugha inayozungumzwa na vijana mtaani.
Sifa za Lugha ya Mtaani
1. Ni lugha legevu isiyozingatia kanuni za kisarufi
2. Huchanganya ndimi
3. Hutumia misimu kwa wingi
4. Hukosa mada maalum
Mfano wa Sajili ya Mtaani
Chali:
Hey, niaje msupaa?
Katosha:
Poa. So, mathee yako alikushow naweza kuja?
Chali:
Ha! Masa hana noma. Si unajua nita...
Katosha:
Chali! Unataka aniletee problem?
Chali:
Mimi ni boy wa maplans. Ngoja nifikirie venye tutamshow
Katosha:
Na by the way, kwani umejipaka mafuta ya manzi. Ama ulikuwa na msichana mgani?
Chali:
Oh! Niliscoop mafuta ya Anita. Si unajua nataka kunukia hmmmm...
Katosha:
Ok. So, umefikiria tumshow nini masa yako? Ama nikona idea poa.
Chali:
Nishow hiyo plot, na by the way, nataka unisaidie kuhusu ile deal yangu na Kaunda. Ile ya siz yangu.
Katosha:
Kwanza tutaplan na huyo siz yako, niwe ndiye nimekuja kuvisit. Mamako atakubali
Chali:
Wow! Idea poa. Utakuwa umekuja kufanya homework. Halafu masa akiishia kwa bed. Homework tutaitupa mbali.
Katosha:
So, utamshow Anita nakuja tufanye homework...
Sajili ya Nyumbani
Hii ni lugha inayotumiwa na watu katika familia. Wanaohusika sana katika mazungumzo ya nyumbani ni mama, baba, watoto, majirani na watu wa ukoo. Maswala yanayorejelewa sana ni yale yanayoiathiri jamii/boma hilo.
Sifa za Sajili ya Nyumbani
Sifa za sajili ya nyumbani hubadilika kulingana na mada inayorejelewa, wanaozungumza na hali katika boma.
Mfano wa sajili ya nyumbani
Baba:
Mama Kadara! Huyo mtoto wako amekuja?
Mama:
Kadara ni mtoto wetu; mimi na wewe.
Baba:
Hapana! Mimi sizai malaya. Huyo ni wako. Hata Bahati ni wako! Hakika wote sita ni wako…
Mama:
Mume wangu unanifanya nikasirike bure tu. Mbona umeanza mafarakano tena.
Baba:
Mafarakano! Mafarakano! Ni mimi niliyekwambia uzae wasichana sita…
Mama:
Lakini sikuzaa pekee. Tulizaa na wewe, mume wangu….
Baba:
Hapana! Uliniona na mimba? Uliniona na maumivu ya uzazi? Umeniona nikinyonyesha mtoto? Mwanamke kuwa na adabu. Nitakurudisha kwa wazazi wakufunze heshima. Na nitaoa sioni tukikaa pamoja.
Mama:
(baada ya kimya) Niambie ulichotaka kuniambia kuhusu Kadara (akijipangusa machozi kwa kitambaa) unajua mume wangu, nakuheshimu. Yangalikuwa mapenzi yangu tungepata wavulana pia. Lakini haya ni mapenzi ya Mungu.
Baba:
Kadara akija umpe kuku apeleke vileoni kwa Mzee Magoti. Nina deni lake kubwa baada ya kunywa tembo siku kadhaa bila kulipa. (akicheka) Hakika hata anastahili mbuzi.
Mama:
Hatuwezi kulipia pombe kwa mbuzi wala kuku. Kuku waliobaki hapa ni wangu na wa watoto wangu. Kuku wako uliwauza.
Baba:
Kelele za chura hazimkatazi ng'ombe kunywa maji. Endelea kupayuka kama wanawake wengine wa kijijini. Nikirudi nikute chakula na maji moto tayari.
Mama:
(akinuna) Haya nimesikia.
Sajili ya Shuleni
Hii ni rejista ya lugha inayopatikana katika mazingira ya shule. Wahusika wake huwa walimu, wazazi na wanafunzi.
Sifa za Sajili ya Shuleni
1. Matumizi ya istilahi (maneno maalum) yanayopatikana katika mazingira ya shule kama vile darasa, mitihani, vitabu, elimu, muhula, masomo
2. Lugha yenye heshima kutokana na utofauti baina ya mwanafunzi na mwalimu, mzazi na mwalimu;
3. Takriri - mbinu ya kurudiarudia maneno. Katika darasa mwalimu hurudia rudia maneno ili kusisitiza anachofunza
4. Ni lugha yenye maswali mengi na majibu. Mwalimu huuliza maswali wakati wa mafunzo. Wanafunzi pia huuliza maswali ili kujua/kupata ufafanuzi.
5. Hutumia lugha ya kukosoana na kurekebishana.
a) Mfano wa Mazungumzo katika Sajili ya Shuleni
Mwalimu:
Mzee Kundu, ningetaka tuzungumze kwa muda kuhusu hali ya mwanao, Machome Kundu.
Mzee:
Machome? Ana nini mwanangu.Kuna nafasi imepatikana ya…
Mwalimu:
Mwanako amebadilika sana kitabia. Alikuwa akifanya vizuri sana katika masomo
Mzee:
Kweli kabisa. Mimi ni mlezi mwema sizai watoto mbu mbu mbu darasani.
Mwalimu:
Ndivyo. Lakini sasa naona ameanza kubadilika. Ameanza kulegea katika mitihani na kuzembea kazini.
Mzee:
Unamaanisha nini? (akiinuka) Inaonekana siku hizi hamjui kuwapa adabu watoto. Ni lazima mtoto wangu amepotoshwa na wengine, katika vikundi vibaya!
Mwalimu:
Hakika, mwanako ndiye anayepotosha wanafunzi wengine. Yeye ni kiongozi wa makundi haramu shuleni, yanayovuruga masomo, kuuza dawa za kulevya na mambo kama haya. Hii ndiyo sababu nimekuita tujadiliane. Ni lazima mienendo hii imechipuka nyumbani.
Mzee:
Ajapo nyumbani, mwanangu huzingatia vitabu pekee hata mamake anaweza kuthibitisha haya. Ikiwa kuna utovu wa nidhamu nina hakika haya yanatoka darasani.
Mwalimu:
Tafadhali keti mzee (akichungulia dirishani) Mtindi! Niitie Machome…
b) Mfano wa Mazungumzo katika Sajili ya Darasani
Mwalimu:
Toeni vitabu vyenu vya Historia mnakili haya. Ni nani atakayetukumbusha tulichosoma wiki jana? Naam Halima!
Halima:
Tulisoma kuhusu Chama cha Mapinduzi
Wanafunzi:
(Wakiinua mikono na kupiga kelele) Mwalimu Mwalimu
Mwalimu:
Inueni mikono nitawaona. Msipige kelele. Halima umenoa. Simama! Mwanafunzi mwengine?
Jadaha:
Tulisoma kuhusu kundi asi la Maji Moto lililopinga wakoloni.
Wanafunzi:
Mwalimu! Mwalimu! Kundi la Maji Maji.
Mwalimu:
Naam mmepata. Lakini nimewaambia msijibu kwa pamoja. Ukitaka kujibu uinue mikono. Jadaha, ni kundi la Maji Maji siyo Maji Moto. Leo tutasoma athari za kundi katika taifa letu la Tanzania na namna lilivyoshindwa nguvu. Lakini kabla hatujaendelea ningependa mniambie, ni matatizo yepi yaliyochochea kuchipuka kwa kundi hilo.
Kirata:
Mwalimu nina swali. Kiongozi wa kundi hilo alikuwa nani?
Mwalimu:
Kirata hukuwa darasani wiki jana. Nione baada ya kipindi hiki. (wanafunzi wakicheka) Nawe wafanyani na kitabu cha Hisabati katika somo la Historia. Kimbia ofisini uniletee kiboko. Ninyi ndio mnaorejesha nyuma darasa langu katika mitihani.
Sajili ya Simu
Hii ni lugha inayotumiwa katika mazungumzo ya simu.
Sifa za lugha ya simu
1. Mazungumzo ya simu ni mafupi, hutumia sentensi fupi zenye muundo rahisi.
2. Hoja hutajwa moja kwa moja bila maneno mengi kwani ili kudhibiti gharama ya simu
3. Huwa na kukatizana kwa maneno kati ya wazugumzaji.
4. Huwa ni mazungumzo baina ya watu wawili pekee; anayepiga na anayepokea.
5. Hutumia istilahi maalum za lugha ya simu kama neno 'hello'
6. Huchanganya ndimi (kutumia maneno yasiyo ya lugha nyinginezo) ili kuwasilisha ujumbe kwa upesi.
7. Ni lugha ya kujibizana.
Mfano wa Sajili ya Simu
Sera:
Hello. Ningependa kuongea na Mika.
Sauti:
Subiri kidogo nimpatie simu.
Sera:
Hello
Mika:
Hello. Sema Sera. Niko kwa mkutano…
Sera:
Pole kwa kukusumbua. Unakumbuka safari yetu ya kesho?
Mika:
Siwezi kusahau. Tunakutana saa ngapi?
Sera:
nampendekeza saa tano machana…
Mika:
Katika Hoteli ya Katata Maa
Sera:
enhe. Hapo kwa heri
Mika:
Haya. Bye!
Maswali.
a)ainisha matawi ya isimu
1.Isimu saikolojia 2.Isimu falsafa 3.Isimu tumizi 4.Isimu tiba 5.Isimu Tiba 6.Isimu Fafanuzi 7.Isimu Jamii 8.Isimu Historia
b)ni nini maana ya fonolojia sintaksia mofolojia semantiki
Fonolojia ni tawi la sayansi ya isimu. Inashughulikia uchunguzi wa mfumo wa sauti katika lugha fulani, kwa mfano ugawanyaji wa irabu na konsonanti. Matokeo ya uchunguzi wa kifonolojia yana umuhimu katika kubuni alfabeti. Dhana ya fonolojia inajipambanua vizuri zaidi ikifasiliwa kwa kutofautishwa na fonetiki. Wakati fonetiki ni taaluma inayochunguza sauti zitamkwazo na binadamu bila kuzihusisha na lugha yoyote, fonolojia huchunguza mfumo wa sauti wa lugha mahususi kama vile sauti za Kiswahili, Kiingereza, Kimwera, na Kinyaturu. ZINGATIA: Fonetiki huchunguza sauti zote zitamkwazo na binadamu; fonolojia huchunguza MFUMO WA SAUTI wa lugha mahususi.
sintaksia ni aina ya sarufi inayojishughulisha na muundo wa maneno katika sentensi.pia hii tawi huhusika uchnganuzi wa aina za maneno,vipashio vya tungo pamoja na aina zake.
semantiki ni tawi la isimu linalojihusisha na uchunguzi na upambanuzi wa maana.ambapo maana inapambanuliwa na kupewa maana kamili au ya msingi. ingawa na maana za ziada huwepo. mfano, neno mama. maana yake ya msingi kabisa ni mzazi wa kike. wakati maana za ziada ni kama vile mtu yeyote ambaye ni mlezi wa familia,pia kama mke wa mtu.
MASWALI
.
a)Fafanua dhana hizi(alama 3)
i)Lafudhi
ii)Krioli
iii)Lahaja
b)Hujambo: You look familiar Nilikuona wapi my friend?
i)Mtindo huu wa kutumia lugha unaitwaje? Eleza (alama 2)
ii)Eleza sababu tatu kutumia mtindo huu wa lugha(alama 3)
iii)Pendekeza njia tatu za kuondoa mtindo huu wa lugha(alama 3)
c) Taja na ueleze sifa tano za lugha ya michezoni (alama 10)
Ni matumizi ya lugha katika muktadha mbalimbali.Kuna sajili anuwai za matumizi ya lugha katika jamii. Hapa tutazingatia mifano michache ya sajili mbali mbali.Kila sajili huwa na sifa mbalimbali zinazoitofautisha sajili hiyo na nyinginezo. Ili kubaini sifa za lugha katika sajili fulani, ni muhimu kuzingatia baadhi ya maswali yafuatayo:
· ni mazungumzo baina ya nani na nani?
· kuna uhusiano gani baina ya wanaozungumza?
· yanapatikana wapi?
· yanatumika katika hali gani?
· yana umuhimu ama lengo gani
· ni istilahi zipi istilahi (maneno maalum) zinazopatikana katika mazingira hayo?
· umaizi wa lugha baina ya wazungumzaji ni wa kiwango gani?
· ni mtindo gani wa lugha unaotumika?
Sajili ya Ajali
Hii ni lugha inayotumiwa katika ambalo ajali imetokea. Wahusika wanaweza kuwa majeruhi, polisi, walioshuhudia au wananchi wengine n.k
Sifa za lugha inayopatikana katika sajili hii
1. Msamiati wa kipekee unaohusiana na ajali kama vile majeruhi, hudumanya kwanza, damu, mkasa.
2. Hutumia lugha ya kudadisi dadisi ili kubaini chanzo cha ajali.
3. Huwa na masimulizi – walio na habari kuhusu kisa hicho hueleza waliyoshuhudia
4. Kutokana na hali ya msukosuko, lugha hii haina utaratibu – watu huwa katika hali ya hofu, kwa juhudi za kuwaokoa majeruhi.
Mfano wa Sajili ya Ajali
Mwanakijiji 1:
Nimesikia twa! Kisha kishindo kikubwa sana (akihema hema) Nikaambia kuna mlipuko tukimbie.
Mwanakijiji 2:
Lilio la muhimu ni kuyaokoa maisha ya majeruhi kwa kuwapa huduma ya kwanza.
Mwanakijiji 1:
Tuondoeni miili ya waliofariki kwanza.
Mwanakijiji 2:
hatuwezi kuishika miili iliyobanwa katika gari hadi polisi wafike. Na ndio hao wanaokuja!
Mwanakijiji 1:
(akikimbia) Ndio hao! Acheni kuiba mafuta! Polisi wanakuja!
Polisi:
Wakitawanya wananchi walioliparamia gari kuiba bidhaa mbali mbali.Liinueni hili gari! Wapi dereva?
Dereva:
(ambaye amelala akihema kwa maumivu, damu ikichuruzika miguuni na mikononi) Nilisitishwa na ng'ombe waliokuwa wakivuka barabara. Nilijsribu kukwepa lakini usukani ukanishinda gari likapoteza mwelekeo…
Abiria:
Alikuwa akiendesha gari kwa kasi sana. Tukampigia kelele apunguze mwendo lakini hakutusikia. Matunda yake…
Mwanakijiji 2:
Niliona gari likibingiria mara kadhaa mpaka likaingia humu mtaroni, ndiyo tukakimbia kuwaokoa.
Polisi:
Nyamazeni! Achieni polisi kazi iliyobaki. Ikiwa kuna yeyote anayejuana na waathiriwa aandamane nasi.
Sajili ya Biashara
Lugha ya biashara huzungumzwa na wauzaji na wanunuzi katika sehemu za kibiashara. Inapaswa ikumbukwe kwamba lugha hii inaweza kubadilika kidogo kulingana na mazingira. Kwa mfano, katika mikutano ya kibiashara, lugha rasmi hutumiwa ilihali katika soko, lugha ya mitaani inaweza kutumika.
Sifa za Lugha ya Biashara
1. Hutumia msamiati wa kibiashara kama vile:
· Fedha
· Faida
· Hasara
· Bei
· Bidhaa
2. Hutumia misimu ili kuwavutia wanunuzi
3. Ni lugha yenye malumbano hasa watu wanapojadiliana kuhusu bei
4. Ni lugha legevu - haizingatii kanuni za lugha.
5. Huchanganya ndimi kwa kuingiza maneno ya lugha za kigeni
6. Ni yenye heshima na unyenyekevu kwa wanunuaji
7. Msamiati katika lugha ya Kibiashara
Mfano wa Sajili ya Biashara
Mtu X:
Tatu kwa mia! Tatu kwa mia! Leo ni bei ya hasara!
Mtu Y:
Unauza hii briefcase kwa pesa ngapi?
Mtu X:
Hiyo ni seventy bob mtu wangu
Mtu Y:
Huwezi kunipunguzia. Niuzie hamsini hivi.
Mtu X:
Haiwezekani mtu wangu. NItapata hasara nikiuza hivyo. Ongeza mkwaja, mama.
Mtu Y:
Basi hamsini na tano.
Mtu X:
Tafadhali ongeza kitu kidogo. Unataka nikule hasara leo? Fikisha sitini na tano.
Mtu Y:
Basi sitanunua hii. Sina pesa hizo zote. Unajua uchumi ni mbaya siku hizi.
Mtu X:
Tafadhali mtu wangu. Huu mkoba ni mzuri sana. Umetoka Germany. Angalia. Unaweka pesa hapa, kitambulisho hapa halafu unafunga hivi. Hauwezi kupoteza chochote ukiwa na mkoba huu. Angalia wewe mwenyewe. Hakuna mahali pengine utaweza kununua mkoba huu kwa bei ghali kama hii.
Mtu Y:
Nimekwambia sina hizo pesa. Nitanunua baadaye ukipunguza bei.
Mtu X:
Lete sixty bob. Lakini utakuwa umeniumiza. Nakufanyia hivyo kwa kuwa wewe ni customer poa.
Mtu Y:
Sawa basi nitanunua. Shika sixty bob.
Mtu X:
Asante Customer. Mungu akubariki. (akimfungia) Hey! Tatu kwa mia. Bei ya hasara! Tatu kwa mia!
Sajili ya Bungeni
Hii ni lugha inayozungumzwa wakati wa kikao cha bunge. Sajili hii ni tofauti na na sajili ya siasa, ambayo huhusisha wanasiasa wakipiga kampeni.
Sifa za Lugha ya Bungeni
1. Ni lugha yenye ushawishi – wabunge hutumia vishawishi ili kuwahimiza wenzao waunge ama kupinga msalaba
2. Ni lugha ya mjadala yenye waungao na wapingao.
3. Ni lugha yenye heshima na nidhamu. Maneno ya heshima kama mheshimiwa, tafadhali na samahani hutumika sana.
4. Hutumia maneno maalum yanayopatikana katika mazingira ya bunge kama vile kikao, mswaada, kuunga mkono, kujadili, kupitisha, n.k.
5. Lugha ya bungeni ni rasmi na sanifu.
6. Hulenga maswala mbalimbali ya kisiasa na maendeleo katika taifa.
7. Huwa na maelezo kamilifu
8. Ni lugha yenye maswali na majibu miongoni mwa wabunge.
Mfano wa sajili ya Bungeni
Spika:
Waheshimiwa, muda unayoyoma. Nawaomba mfanye mazungumzo yenu sauti ya chini tumsikize huyu. Endelea mheshimiwa.
Mbunge 1:
Asante Bwana spika. Hii siyo mara ya kwanza ya kuuwasilisha mswaada huu hapa. Kila mbunge anayethamini raia wa taifa hili ni lazima auunge mkono mswada huu. Katika kikao kilichotangulia, mliupinga mkidai kwamba hauna heshima kwa rais. Leo tumefanya ukarabati wote mliotaka. Hamna budi kuuunga mkono. Bwana spika….
Spika:
Muda wako umekwisha tafadhali keti. Wabunge wataamua hatima ya mswada huu ikiwa utapitishwa kama sheria. Lakini kumbukeni uamuzi wa mwisho ni wa rais
Sajili ya Hospitalini
Hii ni lugha ambayo huzungumzwa katika hospitali baina ya madaktari, wagonjwa, wauguzi n.k
Sifa za Lugha ya Hospitalini
1. Hutumia msamiati wa hospitalini kama vile
· dawa
· magonjwa
· Daktari
· Wadi
· Mgonjwa
· Dawa
· Kipimo
2. Ni lugha yenye upole na heshima
3. Huwa na maswali mengi hasa daktari anapotaka kutambua kiini cha ugonjwa unaomhadhiri mgonjwa wake
4. Ni lugha yenye hofu na huzuni
Mfano wa Sajili ya Hospitalini
Daktari:
Ulianza kuumwa hivi lini?
Mgonjwa:
Kichwa kilianza kuniuma jana jioni baada ya chajio. Nilipoamka asubuhi nikatambua kwamba hata tumbo lilikuwa likiuma pia.
Daktari:
Ulipoanza kuumwa na mwili mzima, ulichukua hatua gani? Hukunywa dawa yoyote?
Mgonjwa:
Nilichukua tembe zilizokuwa zimepatiwa kakangu miaka mitano iliyopita alipokuwa akiumwa na malaria.
Daktari:
Kila ugonjwa huitaji matibabu mbalimbali. Tembe za malaria haziwezi kutumika kutibu maumivu ya kichwa na tumbo. Pia ni hatari kutumia dawa ambazo zimepitwa na wakati. Zinaweza kukuletea madhara zaidi.
Mgonjwa:
(akikohoa) Sijui kama una tembe za kifua pia. Hii baridi inaniletea homa mbaya.
Daktari:
Hatuwezi kukupatia dawa kabla ya kutambua ugonjwa ulio nao. Itabidi tupime joto lako, damu na pia mate yako ili kupata tatizo linalokusumbua. Kisha tutakupatia dawa. Je, una umri wa miaka mingapi?
Mgonjwa:
Nikichukua hizo dawa nitapona?
Daktari:
Matokeo hubadilika kutoka kwa mgonjwa mmoja hadi mwengine. Inaweza kuchukua muda. Huenda ukalazwa kwenye wadi kwa siku mbili tatu hivi. Umri wako, mama?
Sajili ya Kidini
Katika sajili ya kidini tunaangazia lugha inayozungumzwa na waumini/washiriki wa imani fulani wakati wa ibada, sala, katika nyumba takatifu au mahali popote pale ambapo wanazungumzia mambo yanayorejelea imani au Mwenyezi Mungu.
Sifa za Lugha ya Kidini
1. Hutumia msamiati wa kidini kama vile
· Bibilia
· maombi
· mbinguni
· jehanamu
· Madhabahu
· Paradiso
· Mbinguni
· Mwenyezi Mungu
· Mwokozi
2. Ni lugha inayonukuu sana hasa wazungumzaji wanaporejelea Kitabu kitakatifu
3. Lugha yenye heshima, upole na unyenyekevu
4. Lugha sanifu
5. Ni lugha iliyojaa ahadi nyingi kwa wanaoandamana na mafunzo ya kidini na vitisho kwa wanaoenda kinyume na mafundisho
6. Huwa imejaa matumaini
7. Ni lugha yenye kutoa maneno ya sifa, kumtukuza na kumshukuru Mwenyezi Mungu
Mfano wa Sajili ya Kidini
Boriti:
Bwana asifiwe Bi...
Bi Rangile:
Amina, mchungaji. Watoto wanaendeleaje?
Boriti:
Karita hana neno. Mwenyezi Mungu ametunyeshea rehema na neema zake. Je, wajukuu wako wa hali gani?
Bi Rangile:
Wanaendelea vizuri isipokuwa hawataendelea na masomo. Sijui nilimfanyia Mungu dhambi gani.
Boriti:
Nasikitika sana kusikia hivyo. Mungu atawalinda mayatima hao. Yeye ndiye baba wa mayatima. Mungu ni mwenye huruma.
Bi Rangile:
Sijui hayo, mchungaji. Hata sijui maana ya kuishi hapa duniani. Kila siku ni matatizo.
Boriti:
Usife moyo. Mungu anasema katika kitabu cha Yohana 14:18, "Sitawaacha nyinyi kama mayatima..." Kwa hivyo, ukiwa na imani, Mungu atakuonekania.
Bi Rangile:
Basi niombee mchungaji ili Saumu na Neema wapate karo ya kurudi shuleni.
Boriti:
Funga macho tusali. Ewe Rabuka uliyejaa neema na baraka tele. Tunakushukuru na kulitukuza Jina lako takatifu kwa baraka zako za ajabu. Tunajua kwamba wewe ndiye Mungu uliyewatoa wana wa Israeli kutoka Misri. Sisi wenye dhambi tunakuja mbele yako tukiomba ukafanya miujiza katika nyumba hii ya Bi Rangile......
Wote:
Amina.
Sajili ya Kisayansi
Sifa za Lugha katika sajili hii
1. Hutumia msamiati wa kipekee unaoambatana na taaluma inayorejelewa.
2. Huwa na maelezo kwa ukamilifu.
3. Huwa na mpangilio maalum na maendelezo ya hoja na ujumbe.
4. Huchanganya ndimi na kutumia maneno ya kisayansi au lugha mbalimbali.
5. Hutumia lugha sanifu.
6. Ni lugha yenye udadisi mwingi (wakati wa kufanya utafiti)
Kwa sababu zisizoweza kuepukika, kikundi chetu hakitamaliza utafiti ulioratibiwa kukamilishwa mwishoni mwa mwezi ujao. Hii ni kwa sababu ya changamoto kadhaa ambazo tumekutana nazo. Kwanza, viluwiluwi, ambao ndio tunaotafiti wamekuwa haba sana wakati huu wa ukame. Pili, kutokana na kufungwa kwa maabara ya kisayansi katika taasisi hii, ni muhali kufanya majaribio yoyote ya kazi yetu. Tatu, kumekuwa na pingamizi kubwa kutoka kwa baadhi ya wanakijiji kwamba kukusanya viluwiluwi kunawatia hofu. Aidha, tume yetu imepungukiwa na fedha baada ya serikali kusitisha kudhamini utafiti huu.
Baada ya kujadiliana kwa vikao tatu mfululizo, tume yetu inapendekeza haya: Muda wa kufanya utafiti uongezewe kwa kipindi cha miezi sita; serikali kupitia kwa taasisi hii ifadhili wachunguzi. Wananchi wahamasishwe kuhusu umuhimu wa kuwafanyia viwavi utafiti na maabara ya utafiti ikaraatiwe haraka iwezekanayo.
Sajili ya Mahakamani
Hii ni lugha inayozungumzwa na wanasheria, mahakimu, mawakili, washitakiwa na mashahidi katika mahakama.
Sifa za Lugha ya Mahakamani
1. Hutumia msamiati wa kipekee unaorejelea sheria kama vile
· katiba
· sheria
· mashtaka
· Hakimu
· Ushahidi
· Wakili
· Jela
· Mshitakiwa
· Kiongozi wa mashtakiwa
2. Huwa na maelezo marefu na ya kina ili kutafuta ushahidi wowote uliopo
3. Ni lugha yenye kunukuu sana hasa vipengele katika vitabu vya sheria kama vile katiba
4. Ni lugha rasmi na sanifu
5. Ni lugha iliyojaa maswali na majibizano
6. Ni lugha yenye heshima
Mfano wa Sajili ya Mahakamani
Kiongozi:
Musa Kasorogani, mwanaye Bi Safina na Mzee Mpotevu Kasorogani; umeshtakiwa kwa kosa la jaribio la mauaji mnamo tarehe 23/08 mwaka huu. Unaweza kukubali mashitaka, kukana au kunyamaza. Je, unakubali mashitaka.
Musa:
Naomba kukanusha mashtaka hayo, bwana mkubwa.
Kiongozi:
Je, kuna shahidi yeyote katika kesi hii?
Katili:
Hapa mkubwa. Siku hiyo ya tarehe 23/08, Musa alipatikana akiwa akijinyonga usiku wa maneno. Kijiji chote kilikusanyika hapo kwenye boma ya Kasorogani. Nilipoleta polisi, wakamkamata na kumpeleka hospitalini atibiwe kwanza. Ndiposa ameletwa hapa siku ya leo.
Kiongozi:
Je, mshitakiwa una tetesi lolote. Ama pia unaweza kuleta wakili wako azungumze kwa niaba yako.
Kisaka:
Bwana mkubwa, mimi ndiye wakili na shahidi wa Musa. Musa hakuua mtu. Alikuwa akijinyonga kutokana na mkasa uliomfika tarehe hiyo ya Agosti 23 baada ya bibi harusi wake kubadilika. Mimi na mamake, Bi Safina Kasorogani tulijaribu kumtuliza jioni hiyo. Asubuhi nilipoamka siku iliyofuatia, nikapata habari kwamba alikuwa amepelekwa hospitalini. Je, alipojaribu kujiua, alimwua mtu yeyote?
Kiongozi:
Kulingana na katiba ya nchi hii, kifungu cha 12.ab, kuua ni kutoa uhai wa binadamu yeyote. Haijalishi ikiwa ni yeye mwenyewe au ikiwa ni rafiki yake. Hivyo basi jaribio la kujiua ni hatia kulingana na kanuni za nchi hii. Una jingine la kuulizia?
Kisaka:
Je, sheria yetu inaruhusu mtu kuadhibiwa kwa kosa ambalo hakufanya?
Kiongozi:
La hasha.
Kisaka:
Basi tutakuwa tumekiuka kanuni za nchi yetu iwapo tutamhukumu Musa kwa kujiua ilhali hakujiua bado. Tunawezaje kutambua kama angekufa?
Katili:
Inafaa ahukumiwe kinyonga au kifungo cha maisha gerezani. Hata alivunja simu yangu...
Kiongozi:
Order! Lazima kutii mpangilio wa mahakama. Katili hauruhusiwi kuongea bila ruhusa ya hakimu au kiongozi wa mashitaka. Polisi, mpelekeni nje.
Sajili ya Matanga
Ni lugha inayotumiwa katika shughuli za mazishi au nyumbani kwa marehemu.
Sifa za Lugha ya Matanga/Mazishi
1. Hutumia msamiati wa maneno ya huzuni kama vile waombolezaji, makiwa, kifo, mauti, pole n.k.
2. Hutumia lugha ya kuliwaza/kufariji na kupa matumaini hasa kwa waombolezaji.
3. Ni lugha yenye unyenyekevu isiyotumia maneno yanayokera.
4. Hudhihirisha unyonge wa mwanadamu, kama asiye na mamlaka juu ya uhai wake.
5. Huwa na mbinu rejeshi kurejelea maisha ya marehemu alipokuwa hai.
6. Kwa mara nyingi hutumia maneno ya kusifu marehemu kutokana na aliyotenda.
7. Wakati mwingine huwa ni lugha inayodhihiri hali ya kukata tamaa.
Mfano wa Sajili ya Matangani
"Waombolezaji wenzangu, kama mnavyojua tumekusanyika hapa kwa ajili ya kumsindikiza rafiki yetu amabye amelala hapa. Ikiwa kuna mtu alifikwa zaidi na msiba huu ni mimi. Marehemu alikuwa rafiki wangu wa dhati tuliyeshirikiana naye sana. Nilimjua marehemu tukifanya kazi katika soko la Mauzoduni na tangu siku hiyo tumeishi kama ndugu; kuomba radhi ukikosewa; kusaidiana, na kadhalika.
Habari za kifo chake zilinipiga kwa mughdha. Sikuamini kwamba amekufa; kwamba sitamwona tena aushini mwangu. Ninasikitika sana lakini kwa kuwa Mungu hakosi, ninaamini kwamba alimpenda zaidi ya tulivyompenda. Ombi langu kwa Mungu ni moja, kwamba amweke rafiki yangu mahali pema peponi; au popote alipojitafutia siku zake za uhai; nami nitakapokufa anipeleke papo hapo tuendelee kuwa marafiki. Mwenzangu lala. Lala salama tutaonana siku moja"
Sajili ya Michezoni
Lugha ya michezoni hutumiwa wakati wa mashindano ya michezo kama vile kandanda, ukimbiaji n.k Hii inaweza kuwa lugha ya watangazaji/wasimulizi wa mchezo, watazamaji, mashabiki au wachezaji.
Sifa za Lugha ya Michezoni
1. Hutumia msamiati wa kipekee unaohusu michezo kama vile mpira, goli, mchezaji
2. Huchanganya ndimi na kuingiza maneno ya lugha nyingine kama vile Kiingereza. mfano 'goal!!!'
3. Ni lugha ambayo hutumia vihisishi na mshangao kwa wingi
4. Sentensi nyingi katika lugha hii huachwa bila kukamilika hasa hali inapobadilika uwanjani
5. Husimuliwa kwa haraka haraka ili kuambatana na kasi ya mchezo
6. Ni lugha yenye sifa na na chuku kwa mfano msimulizi anaposimulia sifa za mchezaji fulani
7. Hutumia misimu kama vile 'wametoka sare'
8. Hutumia kwa ya kulinganisha ili kuelezea matokeo ya mechi k.m 'walitoka mbili kwa nunge'
9. Ni lugha yenye kukariri (kurudia rudia) hasa mchezaji anapoumiliki mpira kwa muda mrefu au mwanariadha fulani anapoelekea kushinda katika mbio.
10. Huwa na sentensi fupi fupi
Mfano wa Sajili ya Michezoni
Nakwambia ndugu msikilizaji hapa mambo yamechacha kwelikweli. Hawa wachezaji wa Manyuu hawacheki na watu leo. Wameamua kuishambulia timu ya Cheusi bila huruma. Kumbuka kwamba hii ni mara yao ya... Lo! Anauchukua mpira pale, mchezaji nambari tisa... Matiksta. Matiksta, Matiksta na mpira. Anaucharazacharaza pale. Anamwangalia mwenzake. Anaupiga mpira kwa kichwa pale! Lo! Mwenzake anaukosa. Akiushika mpira pale ni mchezaji wa timu ya Cheusi, Romana. Romana, Romana anaelekeza mpira kwenye lango la Manyuu. Anaupiga mpira kwa nguvu! Lo! Hatari sana. Hatari sana katika lango la Manyuu. Hatari! hatari! Goooooooooo ooooh! Wameukosa! Goal keeper ameudaka mpira huo. Pole sana wachezaji wa ... Mlinda lango anaupiga mpira huo kwa hasira. Juu kabisa. Anauchukua pale nambari saba, Saruta. Huyu ni mchezaji machahari sana. Mwaka uliopita, alipewa tuzo la mchezaji bora wa mwaka. Ananyang'anywa na mchezaji mwingine hapa. Wanakabiliana kidogo. Huyu mchezaji anaupiga mpira kwa mguu wa kushoto. Lo! Mpira umekuwa mwingi na ukatoka nje.
Mashabiki wa timu hizi mbili wanasubiri kwa hamu na ghamu kutambua ni nani atakayeibuka mshindi. Katika mechi zilizotangulia, timu hizi zimekuwa zikitoka sare. Lakini leo lazima mshindi atapatikana. Hawa ni fahali wawili. Kumbuka kwamba unapata matangazo haya moja kwa moja kupitia idhaa yako uipendayo, redio nambari moja kote nchini... Mpira unarudishwa uwanjani. Akienda kuurusha pale ni...
Sajili ya Mitaani
Lugha ya mitaani ni lugha inayozungumzwa na vijana mtaani.
Sifa za Lugha ya Mtaani
1. Ni lugha legevu isiyozingatia kanuni za kisarufi
2. Huchanganya ndimi
3. Hutumia misimu kwa wingi
4. Hukosa mada maalum
Mfano wa Sajili ya Mtaani
Chali:
Hey, niaje msupaa?
Katosha:
Poa. So, mathee yako alikushow naweza kuja?
Chali:
Ha! Masa hana noma. Si unajua nita...
Katosha:
Chali! Unataka aniletee problem?
Chali:
Mimi ni boy wa maplans. Ngoja nifikirie venye tutamshow
Katosha:
Na by the way, kwani umejipaka mafuta ya manzi. Ama ulikuwa na msichana mgani?
Chali:
Oh! Niliscoop mafuta ya Anita. Si unajua nataka kunukia hmmmm...
Katosha:
Ok. So, umefikiria tumshow nini masa yako? Ama nikona idea poa.
Chali:
Nishow hiyo plot, na by the way, nataka unisaidie kuhusu ile deal yangu na Kaunda. Ile ya siz yangu.
Katosha:
Kwanza tutaplan na huyo siz yako, niwe ndiye nimekuja kuvisit. Mamako atakubali
Chali:
Wow! Idea poa. Utakuwa umekuja kufanya homework. Halafu masa akiishia kwa bed. Homework tutaitupa mbali.
Katosha:
So, utamshow Anita nakuja tufanye homework...
Sajili ya Nyumbani
Hii ni lugha inayotumiwa na watu katika familia. Wanaohusika sana katika mazungumzo ya nyumbani ni mama, baba, watoto, majirani na watu wa ukoo. Maswala yanayorejelewa sana ni yale yanayoiathiri jamii/boma hilo.
Sifa za Sajili ya Nyumbani
Sifa za sajili ya nyumbani hubadilika kulingana na mada inayorejelewa, wanaozungumza na hali katika boma.
Mfano wa sajili ya nyumbani
Baba:
Mama Kadara! Huyo mtoto wako amekuja?
Mama:
Kadara ni mtoto wetu; mimi na wewe.
Baba:
Hapana! Mimi sizai malaya. Huyo ni wako. Hata Bahati ni wako! Hakika wote sita ni wako…
Mama:
Mume wangu unanifanya nikasirike bure tu. Mbona umeanza mafarakano tena.
Baba:
Mafarakano! Mafarakano! Ni mimi niliyekwambia uzae wasichana sita…
Mama:
Lakini sikuzaa pekee. Tulizaa na wewe, mume wangu….
Baba:
Hapana! Uliniona na mimba? Uliniona na maumivu ya uzazi? Umeniona nikinyonyesha mtoto? Mwanamke kuwa na adabu. Nitakurudisha kwa wazazi wakufunze heshima. Na nitaoa sioni tukikaa pamoja.
Mama:
(baada ya kimya) Niambie ulichotaka kuniambia kuhusu Kadara (akijipangusa machozi kwa kitambaa) unajua mume wangu, nakuheshimu. Yangalikuwa mapenzi yangu tungepata wavulana pia. Lakini haya ni mapenzi ya Mungu.
Baba:
Kadara akija umpe kuku apeleke vileoni kwa Mzee Magoti. Nina deni lake kubwa baada ya kunywa tembo siku kadhaa bila kulipa. (akicheka) Hakika hata anastahili mbuzi.
Mama:
Hatuwezi kulipia pombe kwa mbuzi wala kuku. Kuku waliobaki hapa ni wangu na wa watoto wangu. Kuku wako uliwauza.
Baba:
Kelele za chura hazimkatazi ng'ombe kunywa maji. Endelea kupayuka kama wanawake wengine wa kijijini. Nikirudi nikute chakula na maji moto tayari.
Mama:
(akinuna) Haya nimesikia.
Sajili ya Shuleni
Hii ni rejista ya lugha inayopatikana katika mazingira ya shule. Wahusika wake huwa walimu, wazazi na wanafunzi.
Sifa za Sajili ya Shuleni
1. Matumizi ya istilahi (maneno maalum) yanayopatikana katika mazingira ya shule kama vile darasa, mitihani, vitabu, elimu, muhula, masomo
2. Lugha yenye heshima kutokana na utofauti baina ya mwanafunzi na mwalimu, mzazi na mwalimu;
3. Takriri - mbinu ya kurudiarudia maneno. Katika darasa mwalimu hurudia rudia maneno ili kusisitiza anachofunza
4. Ni lugha yenye maswali mengi na majibu. Mwalimu huuliza maswali wakati wa mafunzo. Wanafunzi pia huuliza maswali ili kujua/kupata ufafanuzi.
5. Hutumia lugha ya kukosoana na kurekebishana.
a) Mfano wa Mazungumzo katika Sajili ya Shuleni
Mwalimu:
Mzee Kundu, ningetaka tuzungumze kwa muda kuhusu hali ya mwanao, Machome Kundu.
Mzee:
Machome? Ana nini mwanangu.Kuna nafasi imepatikana ya…
Mwalimu:
Mwanako amebadilika sana kitabia. Alikuwa akifanya vizuri sana katika masomo
Mzee:
Kweli kabisa. Mimi ni mlezi mwema sizai watoto mbu mbu mbu darasani.
Mwalimu:
Ndivyo. Lakini sasa naona ameanza kubadilika. Ameanza kulegea katika mitihani na kuzembea kazini.
Mzee:
Unamaanisha nini? (akiinuka) Inaonekana siku hizi hamjui kuwapa adabu watoto. Ni lazima mtoto wangu amepotoshwa na wengine, katika vikundi vibaya!
Mwalimu:
Hakika, mwanako ndiye anayepotosha wanafunzi wengine. Yeye ni kiongozi wa makundi haramu shuleni, yanayovuruga masomo, kuuza dawa za kulevya na mambo kama haya. Hii ndiyo sababu nimekuita tujadiliane. Ni lazima mienendo hii imechipuka nyumbani.
Mzee:
Ajapo nyumbani, mwanangu huzingatia vitabu pekee hata mamake anaweza kuthibitisha haya. Ikiwa kuna utovu wa nidhamu nina hakika haya yanatoka darasani.
Mwalimu:
Tafadhali keti mzee (akichungulia dirishani) Mtindi! Niitie Machome…
b) Mfano wa Mazungumzo katika Sajili ya Darasani
Mwalimu:
Toeni vitabu vyenu vya Historia mnakili haya. Ni nani atakayetukumbusha tulichosoma wiki jana? Naam Halima!
Halima:
Tulisoma kuhusu Chama cha Mapinduzi
Wanafunzi:
(Wakiinua mikono na kupiga kelele) Mwalimu Mwalimu
Mwalimu:
Inueni mikono nitawaona. Msipige kelele. Halima umenoa. Simama! Mwanafunzi mwengine?
Jadaha:
Tulisoma kuhusu kundi asi la Maji Moto lililopinga wakoloni.
Wanafunzi:
Mwalimu! Mwalimu! Kundi la Maji Maji.
Mwalimu:
Naam mmepata. Lakini nimewaambia msijibu kwa pamoja. Ukitaka kujibu uinue mikono. Jadaha, ni kundi la Maji Maji siyo Maji Moto. Leo tutasoma athari za kundi katika taifa letu la Tanzania na namna lilivyoshindwa nguvu. Lakini kabla hatujaendelea ningependa mniambie, ni matatizo yepi yaliyochochea kuchipuka kwa kundi hilo.
Kirata:
Mwalimu nina swali. Kiongozi wa kundi hilo alikuwa nani?
Mwalimu:
Kirata hukuwa darasani wiki jana. Nione baada ya kipindi hiki. (wanafunzi wakicheka) Nawe wafanyani na kitabu cha Hisabati katika somo la Historia. Kimbia ofisini uniletee kiboko. Ninyi ndio mnaorejesha nyuma darasa langu katika mitihani.
Sajili ya Simu
Hii ni lugha inayotumiwa katika mazungumzo ya simu.
Sifa za lugha ya simu
1. Mazungumzo ya simu ni mafupi, hutumia sentensi fupi zenye muundo rahisi.
2. Hoja hutajwa moja kwa moja bila maneno mengi kwani ili kudhibiti gharama ya simu
3. Huwa na kukatizana kwa maneno kati ya wazugumzaji.
4. Huwa ni mazungumzo baina ya watu wawili pekee; anayepiga na anayepokea.
5. Hutumia istilahi maalum za lugha ya simu kama neno 'hello'
6. Huchanganya ndimi (kutumia maneno yasiyo ya lugha nyinginezo) ili kuwasilisha ujumbe kwa upesi.
7. Ni lugha ya kujibizana.
Mfano wa Sajili ya Simu
Sera:
Hello. Ningependa kuongea na Mika.
Sauti:
Subiri kidogo nimpatie simu.
Sera:
Hello
Mika:
Hello. Sema Sera. Niko kwa mkutano…
Sera:
Pole kwa kukusumbua. Unakumbuka safari yetu ya kesho?
Mika:
Siwezi kusahau. Tunakutana saa ngapi?
Sera:
nampendekeza saa tano machana…
Mika:
Katika Hoteli ya Katata Maa
Sera:
enhe. Hapo kwa heri
Mika:
Haya. Bye!
Maswali.
a)ainisha matawi ya isimu
1.Isimu saikolojia 2.Isimu falsafa 3.Isimu tumizi 4.Isimu tiba 5.Isimu Tiba 6.Isimu Fafanuzi 7.Isimu Jamii 8.Isimu Historia
b)ni nini maana ya fonolojia sintaksia mofolojia semantiki
Fonolojia ni tawi la sayansi ya isimu. Inashughulikia uchunguzi wa mfumo wa sauti katika lugha fulani, kwa mfano ugawanyaji wa irabu na konsonanti. Matokeo ya uchunguzi wa kifonolojia yana umuhimu katika kubuni alfabeti. Dhana ya fonolojia inajipambanua vizuri zaidi ikifasiliwa kwa kutofautishwa na fonetiki. Wakati fonetiki ni taaluma inayochunguza sauti zitamkwazo na binadamu bila kuzihusisha na lugha yoyote, fonolojia huchunguza mfumo wa sauti wa lugha mahususi kama vile sauti za Kiswahili, Kiingereza, Kimwera, na Kinyaturu. ZINGATIA: Fonetiki huchunguza sauti zote zitamkwazo na binadamu; fonolojia huchunguza MFUMO WA SAUTI wa lugha mahususi.
sintaksia ni aina ya sarufi inayojishughulisha na muundo wa maneno katika sentensi.pia hii tawi huhusika uchnganuzi wa aina za maneno,vipashio vya tungo pamoja na aina zake.
semantiki ni tawi la isimu linalojihusisha na uchunguzi na upambanuzi wa maana.ambapo maana inapambanuliwa na kupewa maana kamili au ya msingi. ingawa na maana za ziada huwepo. mfano, neno mama. maana yake ya msingi kabisa ni mzazi wa kike. wakati maana za ziada ni kama vile mtu yeyote ambaye ni mlezi wa familia,pia kama mke wa mtu.
MASWALI
.
a)Fafanua dhana hizi(alama 3)
i)Lafudhi
ii)Krioli
iii)Lahaja
b)Hujambo: You look familiar Nilikuona wapi my friend?
i)Mtindo huu wa kutumia lugha unaitwaje? Eleza (alama 2)
ii)Eleza sababu tatu kutumia mtindo huu wa lugha(alama 3)
iii)Pendekeza njia tatu za kuondoa mtindo huu wa lugha(alama 3)
c) Taja na ueleze sifa tano za lugha ya michezoni (alama 10)
Tuesday, 26 July 2016
Dhamira katika mashairi ya Kahigi na mulokozi
DHAMIRA KATIKA MASHAIRI YA KAHIGA NA MULOKOZI
K.K. Kahigi na M.M. Mulokozi: Malenga wa Bara
Kitangulizi
Majina ya K.K. Kahigi na M.M. Mulokozi si mageni katika uwanja
wa iasihi ya Kiswahili. Kati ya kazi zao mbalimbali zilizokwishachapishwa za
Mashairi ya Kisasa. (TPH, 1973) Malenga wa Bara (EALB, 1976) na
Kunga za Ushairi na Diwani Yetu (TPH. 1982) ndizo ambazo zimewapa
nafasi muhimu katika dunia ya ushairi wa Kiswahili. Pamoja na hizo, MuIokozi pia
amechapisha tamthilia ya kihistoria inayotumia mawanda ya kiepiki kueleleza
maisha ya shujaa Mkwawa, Mukwawa wa Uhehe (EAPH, 1979) naye Kahigi
akishirikiana na R.A. Ngemera wamechapisha tamthilia ya Mwanzo wa Tufani
(TPH, 1977) yenye kuchambua masuala mabalimbali ya kitabaka katika
jamii. Katika kazi zote hizi waandishi hawa wanashughulikia dhamira kadhaa
zinazohusu nyanja za utamaduni, saisa na uchumi katika maisha ya Watanzania na
Waafrika kwa jumla.
DHAMIRA KUU
Katika diwani yao ya Malenga wa Bara, washairi wamekabili
dhamira mbalimbali, hasa za:
1. Maana ya uhuru
2. Dini na kifo, pamoja na maana ya maisha
3. Kumtetea mkulima na mtu mnyonge
4. Matumizi ya nguvu kama njia ya ukombozi wa wanyonge
5. Mjadala kuhusu masuala ya utamaduni
6. Uzalendo na Wasifu
7. Mapenzi
8. Namna tunavyoishi.
Maana ya Uhuru
Mashairi kadhaa yanachunguza maana ya uhuru. Katika shairi la
kwanza la "Vuteni Makasia," kwa mfano, washairi wanatumia taswira ya safari
kuonyesha kuwa harakati za kutafuta uhuru ni sawa na safari ndefu baharini yenye
matatizo mengi (kupigwa risasi, mbundu za adui, vifo, n. k.).
Tunawaona wavuta makasia (wapigania uhuru) wakifurahia ushindi
baada ya kunusurika na vishindo vya adui:
10. Wakapiga yowe wakifurahika
"Hakika kweli sasa tumeokoka",
11. Na kila mmoja akafikiria
Vipi mke wake atampokea.
Katika shamrashamra hizi za ushangiliaji, wavuta makasia hawa
wanasahau kuwa mwisho wa safari bado. Hii ni tahadhari inayotolewa kuhusu maana
ya uhuru; kuwa uhuru si lelemama, ni mapambano ya kuulinda na kuutetea uhuru huo
pamoja na kuupalilia. Ushindi tuuonao mwanzoni mwa shairi ni ishara tu ya uhuru
wa bendera na wa wimbo wa taifa. Uhuru huu si kamili kama ule wa kiuchumi na
kiutamaduni haujapatikana. Kuangamia kwa wavuta makasia mwishoni mwa shairi ni
ishara ya kuangamia kwa taifa ambalo baada ya kupata uhuru wa mwanzo lilijisahau
likaendelea tu kuusherehekea uhuru huo, bila kuujengea misingi imara ya uchumi,
utamaduni na itikadi sahihi.
Shairi la "Kitu cha Kutamani" (uk. 4), pia linaongelea faida za
uhuru kwa kutueleza juu ya "uhondo" na "tulizo". Hata hivyo washairi
wanasisitiza kuwa mtu apatapo uhuru hana budi kuulinda:
Ni kitu cha kutamani
Cha lazima kwa insani
.....................................
Uhuru ukiupata
Ulinde kwayako mata
Ubeti wa mwisho wa shairi hili nao hali kadhalika unasisitiza
jambo hili kwa kueleza kuwa uhuru sio mwisho wa harakati. Hili limekaziwa pia
katika shairi la "Uhuru" (uk. 14) ambalo limesisitiza kuwa uhuru si kula makombo
hata kama makombo hayo yawe yamenona kiasi gani. Kwa vile shairi hili ni muhimu
na fupi tutalidondoa lote:
1. Ni heri kula karanga, na matunda yenye koko,
Na mapumbaya kusaga, yenye wingi wa mnuko,
Kuiiko kuta kumwaga, uhondo mchanganylko,
Na holi uhuru wako, umekwisha kuuaga.
2. Ni heri kutangatanga, kama moshl wa tambiko,
Bila nyumba yo kujenga, bila sikani la kwako,
Kuliko kuwa na uga, na majumba na majiko,
Na hali uhuru wako, umekwisha kuuaga.
3. Ni heri kuyuga yuga, kwa wele na sekeneko
Kuoza kama uyoga, kufunikwa maumboko
Kuliko kuzidi ninga, uzuri wa mwili wako
Na hali uhwu wako, umekwisha kuuaga.
Katika beti hizi tatu washairi wanaeleza juu ya umuhimu wa mtu
kujitegemea badala ya kutegemea mikopo na "sadaka" zenye kuhatarisha uhuru wake.
Kwa hiyo basi, ni vizuri nchi zijaribu kujitegemea hata kama ni masikini kuliko
kuishi maisha ya kuwa na wafadhili wa nje ambao katika kujidai "kusaidia" hapo
hapo huwa wanazibana nchi hizo ziuze uhuru wao.
Taswira ya safari imerudiwa katika shairi la "Kwenye Safari
Barabarani" (uk. 37) kusisitiza maana ya uhuru ilivyoshikamana na harakati. Hapa
kauli ya "Uhuru ni Kazi" inajidhihirisha, na ubeti wa mwisho unauona uhuru kama
"gogo zito" ambalo linahitaji tahadhari wakati wa kulisukuma. Umuhimu wa
tahadhari hii umejitokeza tena katika shairi la "Mchumba Wangu" (uk. 91). Uhuru
hapa ume-fananishwa na mchumba ambaye bila kuchukuliwa kwa uangalifu huweza
kumgeuka huyo mwenye mchumba pa kumwangamiza. Beti za 9 na 11 zinaoayesha jambo
hili:
9. Hizo pesaze akanza kunihini,
Na kunipokonya zangu kwa uhuni,
Kitwaa kizituma kwao nyumbani,
Sikuweza kuamini!
11. Na nilipotaka kumpa talaka,
Aliita majitu yakanitandika,
Nikapigwa kweli hata nikanyoka,
Sasa siwezi kuwika.
Beti hizi zinaonyesha nguvu za ukoloni mambo-leo, hasa pale
ambapo nchi iliyopata uhuru wa bendera imenaswa na mtego wa ulaghai wa mataifa
ya kibepari. Kupoteza uwezo wa "kuwika" ni ishara ya kupokonywa uhuru wa
kujiamulia mambo. Katika ubeti wa mwisho mshairi anashauriwa kuwa ili
kurekebisha yote hayo nguvu hazina budi kutumiwa:
14. Ndipo hasubiri siku ya lipizi,
Nitetane na yeye huyu jambazi,
Nimtie risasi ya kimapinduzi,
Nikomeshe huu wizi.
Suala hili la matumizi ya nguvu na umwagaji damu tutalipa nafasi
yake ya pekee kwani limezishughulisha sana kalamu za washairi hawa.
Dini, Kifo na Maana ya Maisha
Washairi hawa hawaamini kuwa dini au hata Mungu ana nafasi
yoyote muhimu katika maendeleo ya jamii. Kwa hiyo, mashairi yao yote
yanayoongelea dini, kifo na Mungu yanakejeli na kutufanya tukidharau kifo, na
tusimtegemee Mungu bali tujitegemee wenyewe katika kuleta maendeleo yetu.
Mashairi ya "Tazama Huyo Kipusa" (uk. 6), "Nikifa" (uk. 7), "Saa
ya Mwisho" (uk.10), "Hatima ya Kila Mwali" (uk.22), "Baada ya Matanga" (uk.42),
na "Dawa Mbili" (uk.54) ni mifano ya yale yashughulikiayo kifo kwa kuonyesha
kuwa kufa ni jambo la kawaida, na kwamba hakuna haja ya kusikitishwa sana
nacho.Katika mashairi hayo washairi wameonyesha pia kwamba maisha ni jambo
ambalo kama lilivyo na mwanzo, lazima liwe na mwisho pia. Msichana mzuri
tumwonae katika "Tazama Huyo Kipusa" na "Hatima ya Kila Mwali" twamona mwishowe
akiwa kazeeka na sura yake nzuri ikiwa imechujuka. Taswira hii imetumiwa katika
kuonyesha hatima ya maisha ya mwanadamu.
Kwa washairi hawa kifo ni mwisho wa maisha, na hakuna tena
maisha ya ahera walajehanamu kwani, kama wasemavyo: "Kumbukizi la mkasa, ni
rutuba kuipata."
Washairi hawa wanapopinga udhanifu uliopo katika dini na imani
zilizoegemea kwenye nguvu zilizo nje ya uwezo wa mtu na mazingira yake, hapo
hapo wanamtahadharisha mtu mnyonge, hasa mkulima, kuwa asiamini kwamba unyonge
wake pamoja na shida anazokabiliana nazo hutokana na mambo yaliyoko nje ya uwezo
wake. Jambo hili linachangia katika dhamira ya utetezi wa mtu mnyonge, hususan
mkulima; dhamira inayofuatia karika mjadala wetu.
Kumtetea Mkulima na Mtu Mnyonge
Mashairi ya "Maombolezo ya Mtu Maskini" (uk.15), "Siku Itafika"
(uk.21), "Kauli ya Madhulumu" (uk.33), "Ngonjera" (uk.43), "Vilio vya Dhiki"
(uk.53), "Ni Rahisi Kula Kuliko Kulima" (uk.62) "Mwangalie Mkulima" (uk.67),
"Kilio Kisikikapo" (uk.69), "Sima na Mayai" (uk.70). "Siku Yetu" (uk.90), "Mimba
na Zao Lake Usizaliwe" (uk.94), "Nilipozaliwa" (uk.95), na "Nyimbo za Kijiji" ni
baadhi ya mifano ya mashairi yanayojihusisha na dhamira ya kumtetea mkulima na
mtu mnyonge. Kwa vile haya ni mengi sana katika diwani hii tutachukua machache
kuwa vielelezo.
Shairi la "Maombolezo ya Mtu Maskini" limetumia tamathali nzito
nzito kuonyesha undani wa dhiki za masikini. Linaongelea "panya wa uhitaji",
"simba wa ubepari", "radi ya maradhi", "mishale ya upofu", "shubiri ya ufakiri",
"miiba ya dhuluma" na "funza wa shutuma". Yote haya yamemwandama mtu masikini.
Mtu kama huyu, azaliwapo huwa tayari amekwishaanza kufa. Anaona kuwa haishi bali
yupo tu "kama kitu tu, kama kijiwe tu, kama kijitu tu." Lakmi hata hivyo
washairi hawamkatishi tamaa mtu huyu kwani, kama wasemavyo:
Siku ya wokovu ipo,
Siku ya kukombolewa inakuja!
......................................
Mtu atakuwa mtu
......................................
Na mwanadamu atakuwa huru
Siku hiyo itakapofika mtu mnyonge ataacha "kuwapo na kuanza
kuishi." Lakini, ili ukombozi huu upatikane, harakati lazima ziwepo kwani siku
hiyo ni ya "kitimbanga kuanguka na chamchela kucharuka." Suala hili la mbinu za
wokovu wa mtu huyo mnyonge tutalipatia nafasi ya pekee katika mjadala wetu kwani
nalo pia limewashughulisha sana Kahigi na Mulokozi.
Katika "Ngonjera", Mulokozi ameshughulikia mgogoro wa maisha ya
mtu mnyonge na kuyatolea suluhisho. Misingi ya suluhisho hili ni zao la athari
za Azimio la Arusha, ndiyo sababu linaishia na wito wa kurudi kijijini:
KIJANA:
|
Sasa sitasitasila
| |
Nitakwenda kwa haraka, furaha kuitafuta,
| ||
Kisimanimwa baraka, shamba kulikotakata!
|
Ijapokuwa kwa nyakati hizi suluhisho hili la kuwarudisha
vijijini watu walioshindwa na maisha mjini ni jawabu linaloonekana kupwaya,
katika miaka ya mwisho ya sitini na ya mwanzo ya sabini lilikuwa na misingi
kwani nguvu za Azimio la Arusha bado zilikuwa na vuguvugu kubwa, na imani za
watu katika vijiji, hasa vijiji vya ujamaa, bado zilikuwa juu sana.
Shairi la "Mwangalie Mkulima" linatoa taswira ya hali duni mno
ya mkulima ambaye, twaelezwa, katika jitihada zake za kupasua "udongo na
miamba", mwishowe unaambulia kibaba tu. Taswira hii imewekwa sambamba na za watu
wengine kama vile "kiongozi na tumbole", "Singh na jiduka lake" oa "mtoto
rijale" mwenye benzi ambalo hakulitaabikia. Kwa hiyo upande mmoja wako hao wenye
vyao, na upande mwingine yuko mkulima na kuli wenye kutiririsha jasho
kuwashibisha hao wa kundi la kwanza. Ubeti wa mwisho wa shairi hili unaungana na
mashairi yahusuyo uhuru ambayo tumeyaangalia:
7. Naam watawme wote na kisha,
Tafiti tena ramaniya maisha:
Shangwe za uhuru sasa zimekwisha,
Kilichosalia kejeli komesha!
Kejeli wanayotaja washairi hapa ni kuwa badala ya uhuru kuleta
usawa baina ya watu katika jamii, utabaka umeendelea na masikini wamezidi
kufukarika wakati matajiri nao wameendelea kutajirika. Jambo hili limesisitizwa
pia katika shairi la "Sima na Mayai" ambalo linaonyesha jinsi ambavyo hali ya
mkulima mwenye kutoa mchango mkubwa katika elimu ya vijana imebaki kuwa duni
wakati ambapo hali za wasomi hao zimebadilika na kuwa nzuri. Maisha ya raha na
starehe tuyaonayo katika beti za 1, 3, 5, 7, 9 na 11 yanaashiria ukuta uliopo
baina ya waliobahatika kupata elimu ambayo imekuwa daraja la kuwavusha hadi
ng'ambo ya pili yenye uhondo wa kiuchumi; na yale ya beti za 2, 4, 6, 8, 10, 12,
13, 14, 15 na 16 ambayo ni ya umasikini hohehahe. Hapa basi, dhamira ya elimu na
nafasi yake katika jamii inajidhihirisha: elimu hiyo bado haijawa chombo cha
wokovu wa wanyonge.
Beti za 15, 16 na 17 zenye kuonyesha uzee na ubovu wa mwili wa
mkulima hapo hapo zinaasa kuwa kuna haja kama si kumlipa mkulima kwa kujitolea
kwake muhanga katika kuwaelimisha vijana, walau asiachwe
Kufia kando ya njia
Kama mwanamke mgumba
Kama kokwa lisilo na mbegu
Mkulima anayechangia sana katika kulielimisha taifa ni sawa na
"mgomba wenye mkungu bora", mgomba ambao hauna budi kuwekewa mhimili ili
ujiegemeze juu yake. Huu ni wito wa kuwalipa wakulima kwa elimu waliyopatia
jamii.
Hali duni ya maisha ya mkulima imesawiriwa pia katika "Nyimbo za
Kijiji "ambazo zinaonyesha jinsi mvua zilivyochelewa na vile ambavyo "mtama
umemalizwa na ndege." Hata hivyo, shairi la "Weka Jembe Mpini" linaleta
matumaini mema katikati ya dhiki za mkulima ijapokuwa hatuonyeshwi hasa namna
mabadiliko yaonekanayo yanavyopatikana.
Matumizi ya Nguvu kama Njia ya Wokovu wa Wanyonge
Suala la utatuzi wa migogoro inayoshughulikiwa na wasanii katika
kazi za fasihi lina nafasi muhimu sana wakati wa kuchambua kazi hizo. Wakati
ambapo akina Kahigi na Mulokozi wamejihusisha sana na migogoro ya kijamii, na
hata kushauri kuwa baadhi yake huweza kutatuliwa kwa kuthamini na kuendeleza
kilimo, washairi hawa wanaelekea kusisitiza kuwa NGUVU na kumwaga damu ni lazima
ili kuleta wokovu wa mtu mnyonge. Kwa hiyo basi, tunakutana na mashairi kadhaa
yanayosisitiza jambo hili katika Malenga wa Bara. Mathalani, katika
shairi la "Siku Itafika" (uk.21), washairi wanatuambia:
4. Siku hiyo itafika, itafika, itafika,
Vilio vitasikika, beberu asononeka,
Damu zitatiririka, dhalimu kuhasirika...
Ili "siku hiyo" ya wokovu wa wanyonge ifike, washairi wanatoa
wito katika shairi lao la "Njiaya Damu" (uk.32):
Wito unaita: "Shikeni mikuki
Mapanga na miundu na bunduki
Mwende kwenye kituo cha uhaki"
Kwa hiyo basi, kwa Kahigi na Mulokozi haki itapatikana kwa
kupitia mtutu wa bunduki, ndiyo maana wanasisitiza katika shairi hilo hilo:
Ninaona bahari kubwa ya damu
Bali najua kutoka kwenye damu
Patazuka maisha mastakimu
Itashere'ka ya uhuru mizimu.
Mkabala huu wa kuuona umwagaji damu kuwa ndilo jawabu la kuleta
haki na usawa baina ya watu unajitokeza katika mashairi ya "Mtokoto" (uk.35),
"ViliovyaDhiki" (uk.53), "Inuka" (uk.55), "Siku za Bunduki" (uk.56), "Ni Rahisi
Kula Kuliko Kulima" (uk.63), "Fundo Kusukasuka" (uk.65). "Siku Yetu" (uk.91),
"Mchumba Wangu" (uk.93), "Nilipozaliwa" (uk.96), "Namna Tunavyoishi" (kurasa za
105 · 108) na "Zama Hizi" (hasa ukurasa wa 115).
Mashairi mengine ni "Namna Tunavyoishi" na "Zama Hizi" ambayo tutayachambua
kipekee baadaye.
Kwa baadhi kubwa ya wasomaji, inawezekana kuwa ushairi wa
umuhimu wa utumiaji nguvu na umwagaji damu katika kuleta wokovu wa wanyonge
utaonekana kuwa wa kijaziba mno (amachist); na kubakia kuwa ni
umwagaji damu kwa ajili tu ya umwagaji damu. Hata hivyo kuna mistari miwili ya
mashairi mawili tofauti ambayo inaonyesha dhahiri kuwa siyo nia ya washairi
kuuchukulia umwagaji damu kijuujuu tu. Mstari wa kwanza wa "Nipe Mwongozo"
(uk.93) unasema: "Nipe mwongozo haraka, na kikoba cha baruti."
Kwa hiyo siyo suala la baruti na bunduki tu bali lazima harakati
hizo ziwe na mwongozo kamili. Jambo hili limerudiwa katika mstari wa mwisho wa
shairi la "Maombolezo ya Mtu Maskini" ambamo twaelezwa kuwa siku itakapowadia ya
"kitimbanga kuanguka" ili mtu mnyonge aache kuwapo na aanze kuishi, hapo ndipo:
Kila mtu ataishi
Na bunduki begani, jembe mkononi
Na kitabu mfukoni.
Kwa kututolea vitu hivyo vitatu: bunduki, jembe na kitabu,
washairi wanadhihirisha kuwa matumizi ya nguvu kama njia ya ukombozi wa mtu
mnyonge hayana budi kuambatana na ufanyaji kazi pamoja na kuwa na mwongozo
kamili.
Hata hivyo, maswali kadhaa yanazuka kuhusu dhamira hii. Je,
matunuzi hayo ni dhidi ya nani hasa katika jamii kama ya Tanzania? Nani
watashika hizo bunduki? Chini ya uongozi wa nani? Watazitoa wapi?
Mjadala Kuhusu Masuala ya Utamaduni
Kuanzia miaka ya sitini na tano hadi katikati ya miaka ya sabini
kulikuwa na vuguvugu la kiutamaduni katika nchi za Afrika. Hii ilikuwa miaka ya
Waafrika kujizatiti na hata kuusisitiza Uafrika wao baada ya mkoloni kuondoka.
Mawazo ya kusisitiza Uafrika (Negritude) yalipata msisitizo mpya, na hata kwa
upande wa siasa itikadi mbalimbali zilianza kutafutiwa misingi ya Uafrika:
kukazuka "usoshalisti wa Kiafrika", "Ujamaa; nakadhalika.
Kwa upande wa masuala ya utamaduni katika Afrika ya Mashariki,
mjadala ulioanzishwa na Okot pBitek katika utungo mrefu wa Wimbo waLawino
(EAPH, 1975) ulisambaa haraka mno mithili ya moto katika mbuga kavu. Cheche za
moto huu za kuutetea utamaduni wa Mwafrika zimejitokeza hapa na pale katika
diwani hii ya Malenga wa Bara.
Shairi la "Kwa Shaaban Robert" (uk.5) ambalo ni la kitawasifu,
papo hapo linatukuza lugha ya Kiswahili, na lile la "Zuka" (uk. 7) linatoa wito
wa kufufua utamaduni wa Mwafrika:
Zuka uwke mzuka,
Utamaduni Afrika!
Yule aliyekuteka
Hatarudi kukuteka!
................................
Zuka, Utathaminika
Zuka, utakumbatika.
Katika kusisitiza umuhimu wa kujirudishia hadhi kwa Mwafrika,
washairi wanasisitiza-pia umuhimu wa kuchuja katika ujenzi wa utamaduni mpya:
Chuja, uchuje, mchuja
Utamaduni wa tija
Kumbata ule wa haja
Usikumbate vioja;
Kasumba inayofuja,
Hamna haja kuonja!
Kasumba wanazozipinga washairi hapa ni zile zile anazozikemea
Lawino anapomshauri mume wake arudie utamaduni wao badala ya kukumbatia
kikasumba tamaduni za nje.
Shairi la "Kitu Nisichokitaka" (uk.10) nalo linawekea mkazo
umuhimu wa mtu kuwa na uasili katika utamaduni wake badala ya kuvaa tamaduni za
nje zenye kumfanya aooekane kama mwenye nguo iliyojaaviraka. Shairi la "Wimbo
Uliosahaulika" (uk.87) haU kadhalika linasuta kuabudu mambo ya nje: kuanzia
"mitishamba ya kigeni inayoukwajua mwili wangu" - hapa ikamaanisha madawa ya
kigeni kama vile Ambi wanayotumia baadhi ya Waafrika ili kujaribu
kuiondoa "aibu" ya weusi wa ngozi zao na kuwafanya wawe weupe kama Wazungu -
pamoja na "utumwa (wa) talasimu za kigeni shingoni.../na mizimu
nisiyoijua...," mambo ambayo yanaashiria dini na imani ngeni zinazomfanya
Mwafrika awe mtumwa wa mawazo nchini mwake. Beti za 4, 5, 6 na 7 za shairi hili
zinatoa uamuzi wa hatua za kuchukuliwa katika kurudia utamaduni wa Mwafrika na
kutupilia mbali kujidharau.
Japokuwa dhamira kuu katika shairi la "Mlima wa Kimombo" (uk.97)
ni ile ihusuyo aina ya elimu itolewayo katika jamii, washairi pia wameihusisha
dhamira hiyo na masuala ya utamaduni, kwani katika elimu hii kuna kuvaa "pekosi
kike, Nywele za wafu, Kucha za damu." Haya ndiyo yale yale anayoyapiga vita
Lawino dhidi ya akina "Klementina'' wa Afrika.
Kwa jumla tunaweza kusema kuwa mashairi yote ambayo
yamejishughulisha na masuala ya utamaduni katika diwani hii, hapohapo yameungana
na yale yaelezayo maana ya uhuru kwani sehemu mojawapo muhimu ya uhuru wa mtu
inahusu kuthamini na kuuamini utamaduni wake.
Uzalendo na Wasifu
Uzalendo ni mapenzi ya mtu kwa nchi yake; ni kipimo cha yale
mapenzi aliyo nayo mtu kwa wanajamii wenzake. Kwa maana hiyo ya harakaharaka
basi, itadhihirika wazi kuwa "uzalendo" wauonyeshao Kahigi na Mulokozi katika
diwani ya Malenga wa Bara umepevuka zaidi ya ule wa Mashairi ya
Kisasa uliokuwa wa kuisifu tu nchi katika ukubwa wake: mapenzi yasiyo na
welekeo wowote (angalia kwa mfano mashairi ya "Nitaisifu Tanzania" na "Nakuahidi
Tanzania")
Mashairi ya "Kwa Shaaban Robert" (uk.5) "Sudi ya Tanzania"
(uk.36), "Nchi Yangu Utadiriki" (uk.80) na "Kiswahili" (uk.84), ni ya wasifu na
kizalendo, na hapohapo yanamtetea mtu mnyonge. Haya yanaungana na yale ya
kumtetea mkulima na masikini, na kudhihirisha kwamba dhana ya uzalendo ni suala
la kitabaka. Mtu hawezi kuipenda nchi tu katika ukubwa wake bila kuelekeza hisia
zake za mapenzi kwa tabaka fulani katika nchi hiyo. Kwa mfano, katika shairi la
"Nchi Yangu Utadiriki", zaidi ya kuonyesha mapenzi yao kwa Tanzania, hapohapo
washairi wanasisitiza kuhusu mapinduzi yatakayowainua makabwela baada ya
kuzinduka na kutambua uhalisi wa utabaka wa jamii katika ubeti wa mwisho:
Tanzania utadiriki
Kwa taayo ya mapinduzi,
.......................................
Watazinduka makabwela,
Watainuka makabwela,
Zitakatweni silisila!
Uzalendo wa akina Kahigi na Mulokozi, basi, si ule wa kuipenda
nchi kwa ajili ya kuipenda tu, bali umeelekezwa kwa tabaka la wanyonge kama vile
makabwela.
Mapenzi
Robo nzima ya kitabu cha Mashairi ya Kisasa ni ya
mashairi ya mapenzi baina ya wavulana na wasichana; mapenzi ya "sili silali".
Ijapokuwa hapa na pale ile hali ya "sili silali" inaibuka katika Malenga wa
Bara, washairi wamepunguza sana idadi ya mashairi ya mapenzi ya namna hiyo.
Wakati ambapo mashairi ya "Barua Kwa..." (uk.39), "Wimbo Kabla ya Kulala"
(uk.79), na "Mapenzi" ni ya kuonyesha tu hisia za mtu kwa mpenzi wake, yale ya
"Sifa Zako Nitataja" (uk.24) na "Asali ya Nyuki" (uk.83) japokuwa ni ya mapenzi
pia, yanatoa ujumbe wenye kupevuka zaidi ya ule wa "sili silali". Kwa mfano
katika "Sifa Zako Nitataja", baada ya sifa mzo mzo ambazo zimetolewa kuhusu
mpenzi mwenye umbo na sura nzuri sana, tunajulishwa kuwa jina la mpenzi huyo ni
Kapesa. Jina hili linatupa maana nyingine ya shairi hili ambayo inaungana
na ile ya dhamira ya fedha inavyoabudiwa katika jamii.
Namna Tunavyoishi
Yako mashairi mawili katika Malenga wa Bara ambayo ni
muhimu sana kwani yanatoa taswira ya maisha yalivyo katika jamii yetu nyakati
hizi. Hayo ni "Namna Tunavyoishi" (uk. 105) na "Zama Hizi" (uk. 113). Kwa vile
haya yana umuhimu wake, uchambuzi tutakaofanya wa mashairi haya, hasa wa lile la
"Namna Tunavyoishi", utafuata ubeti hadi ubeti; au walau utazingatia mafungu ya
beti zenye kushirikiana.
Beti mbili za kwanza za shairi la "Namna Tunavyoishi" zinauliza
maana ya uhuru na pia maana ya maisha hasa pale ambapo "uhuru" na maisha hayo
yamezungukwa na taabu, vilio, afya mbaya, na watu ambao hawaishi bali wanadumu
tu. Taswira hii ya dhiki imesisitizwa katika beti za tatu na nne ambazo
zinaeleza jinsi maradhi mbalimbali yalivyoenea katika jamii. Beti za tano hadi
kumi na moja zinaonyesha kuwa badala ya kukaa na kulalamikia dhiki, watu
wanyonge hawana budi kuharakatika. Washairi wanaziona harakati hizi kuwa sawa na
safari juu ya barabara iliyo na kokoto. Wanasema:
Na katika kupigana, hutokea tukakonda
Ya kokoto kalisana, barabara ina nunda
Lakini wanasisitiza kuwa kwa vile umma wa watu hauwezi kukaa tu
na kuvumilia dhiki ziletwazo na "zimwi na vifutu" (viongozi wapotofu), basi
nguvu lazima itumiwe ili kuleta mabadiliko yanayotakiwa, kwani, kama wasemavyo
wenyewe:
Maisha ni harakati, mazingira kuyadhidi
Hajaya kunyonya titi, la uhai kufaidi
Na mtu kila wakati, budi awekejuhudi
Lau kwenye harakati, atashindwa na hashindi.
Katika kuyaangalia maisha ya leo, washairi wameonyesha uzuri na
ubaya wa maisha hayo; lakini wamesisitiza ile dhamira ambayo imewashughulisha
sana katika ushairi wao: kwamba uhuru si sherehe zisizo na mwisho. Maisha ya leo
hayajatufikisha mahali pa kusherehekea:
Haujajiri wakati, wa mtu kushereheka
Akalinyonya na titi, kwa raha kufaidika
Kilasiku harakati, zinazidi kucharuka
Kinyume na E. Kezilahabi katika diwani yake ya Kichomi
(Heinemann, 1974) ambamo mashairi yake mengi yanakatisha tamaa, Kahigi na
Mulokozi katika Malenga wa Bara, na hasa katika shairi hili la "Namna
Tunavyoishi", wamesisitiza kuwa ushindi wa watu wanyonge hauna budi kupatikana
kwani lazima "kule mbele kupateka."
Kwa Kahigi na Mulokozi, dunia ya leo imezungukwa na uovu na uozo
mwingi sana ambao lazima upigwe vita japokuwa baadhi ya mafundisho ya dini hudai
kuwa mabaya yote yatalipizwa siku ya kiyama. Wanasema:
Japo Dini zimezuwa, etimoto utazima
Bali sisi tunajuwa, kuwa hakuna kiyama
Mwanga wa moto muruwa, hakuna wa kuuzima.
Kwa washairi hawa, zama zetu bado si za uhuru kamili, ndiyo
maana shairi linamalizia na wito wa kusimama imara kuuwania uhuru ili kuangamiza
dhiki na kuleta "ngoma mpya ya dunia."
Maudhui ya shairi la "Zama Hizi" yanalandana sana na ya shairi
la "Namna Tunavyoishi". Shairi linasisitiza kuwa dhiki zimekithiri, magonjwa
yamesambaa, na uhuru si uhuru kamwe: hata ule "uhuru" uliopatikana mwanzo
umetekwa nyara huku wale walioshiriki katika kuupigania wanaendelea na maisha
duni:
Sasa asaliya Uhuru yaliwa na kiboko wa inda,
Na mashujaa wajana walamba midomo mikavu
Kote kuna vilio vya nyasi na miti inayoungua
Dhamire Nyinginezo
Katika kuchambua dhamira mbalimbali zinazojitokeza katika
Malenga wa Bara tumeorodhesha mashairi kadhaa kwa kila dhamira. Mashairi
hayo yanawakilisha tu orodha ndefu zaidi, na ni juu ya msomaji kuyaangalia yale
ambayo hayajaorodheshwa na kujaribu kuyachambua na kuyaainisha.
Hata hivyo, hapa tutaangalia baadhi ya mashairi mengineyo ambayo
kidhamira yanajitegemea.
Shairi la "Jua la Dhahabu" (uk.18) linaongelea Azimio la Arusha
na jinsi ambavyo, sawa na jua,
Miali yake imepenya
Anga la nchi yangu
Na kukifukuw kiw
Kiza kinachoongelewa hapa ni ubepari na unyonyaji ambao ulipigwa
vita na Azimio la Arusha. Jua hili linatakiwa liwake ili liwamulikie wanyongc
vidato vya kupandia kuelekea kwenye neema na maendeleo yatakayowasha tabasamu
katika mioyo yao. Nguvu hizi za Azimio zimeelezwa pia katika shairi la "Ngoma ya
Radi" (uk.110) ambalo Umeonyesha jinsi ngoma hiyo ilivyowazindua wanyonge.
Kati ya mashairi yote ya diwani hii, shairi ambalo linaonekana
limekosa welekeo, halina kichwa wala miguu, ni lile la "Vita" (uk.l9) lenye beti
zote ishirini na mbili zikishangilia vita ambavyo hatuelezwi ni vya nani, bali
kupewa tu vidokezo vinavyopwaya katika ubeti wa pili na wa tatu vyenye kugusia
kuwa vita hivi ni vya watu ambao,
Bezo wamepita
Kwonyesha wataka, kuwasio duni
Kwonyesha hakika, kuwa si manyani
Vidokezo hivi havitoshi kutueleza kwa hakika kama vita hivi ni
vya kumpigania nani hasa.
Shairi la "Buyu la Kaya Limevunjika" (uk.29) ni la maombolezo na
kilio cha watoto kwa kutokwa na mama yao. "Buyu la kaya" ni ishara ya shibe na
uhai, kwani aghalabu buyu hutunzia maziwa ambayo hupendwa sana na watoto. Lakini
pia katika shairi hili nafasi, na hata dhana ya mama katika familia imeelezwa.
Twaelezwa kuwa wakati mama alipokuwa hai nyumba ilikuwa inang'ara na kunukia.
Ila:
Sasa uchafu umetanda, mnuko umechacha
Na haipo furaha,
Shairi hili basi, linaonyesha kuwa nyumba bila mama si nyumba:
ni mahame ambamo hamna uhai, furaha wala raha.
Shairi la "Soga" (uk. 85) - shairi ambalo linatumia sana ucheshi
katika kuyatoa maudhui yake - linaasa kuwa kila hali na kila kitu kina pande kuu
mbili, na kusisitiza dhamira ya nguvu za pesa katika jamii. Washairi wanasema:
Na dunia ni mfuko na nchi zote ni masoko!
Fedha ndiyo bwana, fedha ndiyo Mungu
Anayekanusha hamjui Mungu!
Washairi wameamua kumalizia diwani yao kwa shairi lenye kuleta
matumaini kwa wanyonge. Shairi la "Siku Imefika" (uk.120) linaeleza jinsi
ukoloni wa Mreno ulivyoangushwa, na jinsi kaburu anavyopapatika kutokana na
harakati za ukombozi. Ni shairi la nderemo, chereko-chereko na la kuleta
matumaini mema kwa wote wanaonyonywa, wanaonyanyaswa na kuonewa.
MATUMIZI YA BAADHI YA VIPENGELE VYA FANI
Katika kuzichambua dhamira mbalimbali za Malenga wa Bara,
kila mara tumekuwa tukigusia pia masuala ya fani. Kwa mfano, katika kuiangalia
dhamira ya "Maana ya Uhuru" tulitaja jinsi taswira ya safari ilivyotumika
kueleza dhana ya uhuru. Mashairi ya "Vuteni Makasia", "Kwenye Safari
Barabarani", "Msafiri Mpya" (uk.40), na "Kauli ya Mzee" (uk. 22) yametumia pia
kipengele cha fani cha taswira ya safari kutolea maudhui yake yahusuyo
harakati za ukombozi za kujitafutia uhuru kamili. Vipengele vingine vikuu vya
fani walivyotumia Kahigi na Mulokozi katika diwani yao ni:
1. Tamathali za semi
2. Misemo, methali na nahau
3. ishara ya ngoma
4. Taswira za usambamba
5. Majigambo
6. Mtindo wa tambo
7. Mtindowavinanamizani.
Tamathali za Semi
Tamathali za semi zimetumiwa katika mashairi mengi humu
kutajirisha maudhui, na pia kuleta picha kamili ya lile wanaloiieleza washairi.
Mathalani, katika sbairi la "Vuteni Makasia" tunaelezwa hivi
kuhusu mwendo wa mashua:
9. Mashua ikenda ikichachamaa
Uso wa bahari ikiuchubua
Hii ni tashihisi, kwani, kama tujuavyo bahari haina uso uwezao
kuchubuliwa, bali uso huu ni wa kuwazika tu.
Shairi la "Maombolezo ya Mtu Masikini" limejazana tamathaii
zenye kuonyesha undani wa dhiki za mtu masikini kama vile "panya wa uhitaji",
"simba wa ubeberu", "matiti ya uwingu wenye ubahili". Yote haya yamesaidia
kueleza vizuri zaidi dhiki hizo kuliko vile ambavyo ingekuwa kama washairi
wangetumia maneno kama vile "ubeberu mbaya", "maradhi mengi", na kadhalika,
ambayo ni ya kawaida mno.
Katika shairi la "Sima na Mayai" mzazi anamuasa kijana wake kwa
njia ya tamadhali asemapo:
16. Usiniache kufw kando ya njia
Kama mwanamke mgumba
Usiniache ning'oke kamo muyombo
Usio na mzizi wa hati
Tamathali ya tashbiha imetumika - hapa kusisitiza umuhimu wa
wasomi kuwahudumia wale wahowasomesha. "Mwanamke mgumba." "kokwa lisilo na
mbegu" na "muyombo usio na mzizi wa kati" ni ishara za viumbe wasio au visivyo
na uwezo wa kuendeleza uhai duniani. Mzazi anayelalamika katika shairi hili
wakati huohuo anamdai kijana wake kuwa yeye si nigumba, si kokwa lisilo na mbegu
wala si muyombo usio na mzizi wa kati kwani tayari ameshadhihirisha uwezo
wake wa kuendeleza maisha kwa kumzaa kijana huyo msomi. Uwezo huo pia tunaweza
kuuchukulia kiishara kuwa ni kule kujitolea kwa mzazi au jamii kuwasomesha
vijana.
Mfano mwingine wa matumizi ya tamathali umo katika shairi la
"Kwa Shaaban Robert" ambako twaelezwa kuwa maandishi yake ya kudumu yanakata
"kama panga.''
Ni dhahiri kuwa iko mifano mingi mingine ya tamathalt za semi
katika diwani hii ambayo wasomaji huweza kuitafiti na kuigundua wenyewe.
Misemo, Methali na Nahau
Mashairi kadhaa katika diwani hii yametumia misemo, methali na
nahau si kama njia ya kupamba tu bali pia katika kutajirisha yale
yanayoongelewa.
Mathalani, katika shairi la "Saa ya Mwisho, (uk. 10) msemo wa
"Nguvu huvunjwa na pesa" umetumiwa kuonyesha nguvu za pesa katika jamii.
Shairi la "Mlima wa Kimombo" nalo limetumia methali kadhaa kuwa
njia ya jadi ya kupinga kukumbatia utamaduni wa kigeni bila kuchuja. Misemo na
methali kama "Mtoto mwenye njaa haonyeshwi titi," "Muwinda ndege huzunguka
apajue mahali mtama ulipomalizwa na ndege," "Utokapo nje huwa kware," "Uzuri wa
tunda la mtwetwe ndani limeoza," "Anayekohoa na kutema huwa anapunguza ugonjwa,"
"Mto unaotiririka haurudi nyuma," na kadbalika; ni raifano mizuri ya pamna
misemo na methali vinavyotumiwa kuyajenga maudhui. Kwa mfano, katika methali ya
"Mto unaotiririka haurudi nyuma" kuna fundisho la kutokukata tamaa katika
harakati za kujikomboa; fundisho ambalo ndani yake pia lipo tumaini la ushindi.
Ishara ya Ngoma
Katika baadhi kubwa ya jamii za Afrika, ngoma hutumika kwa wito
au kwa ajili ya vifijo na hoihoi za ushangiliaji.
Katika Malenga wa Bara, ngoma imetumika kwa makusudi hayo
hayo. Katika shairi la "Kwenye Safari Barabarani", kwa mfano, washairi wanasema:
10. Najinsi tuendeavyo lengo lile,
Ndivyo jinsi ngoma zetu lelelele,
Ziongezavyo mipwito ya kelele
Kelele zizochangamana rajua.
Mipwito hii ya ngoma ni ishara ya ushindi ambao hauna budi
kupatikana katika vita vya ukombozi wa watu wanyonge.
Shairi la "Sherehe" (uk.49) pia limetaja ngoma katika beti zake
nyingi likieleza jinsi "ngoma mafungu mafungu" zitakavyochezwa katika sherehe
hii (ambayo hata hivyo, hatuoni msingi wake). Ni sherehe, vicheko, vifijo na
ushangiliaji wa jambo ambalo washairi hawatuonyeshi kinagaubaga kuwa ni jambo
gani.
Mstari wa mwisho kabisa wa shairi la "Namna Tunavyoishi",
unasema: "Kwa sababu haisiti, ngoma mpya ya dunia." Hii "ngoma mpya ya dunia,"
sawa na ile tuikutayo katika shairi la "Ngoma ya Radi", ni tangazo la maisha
mapya; ni mbiu ya mgambo kuhusu maisha ya usawa, haki na upendo baina ya watu
watakapojikomboa.
Taswira za Usambamba au Ulinganishi
Taswira ziitwazo za usambamba au za ulinganishi ni zile ambazo
hutupa nyuso mbili za jambo katika kujenga maudhui fulani. Kwa mfano, katika
riwaya ya Kasri ya Mwinyi Fuad, (TPH, 1974) taswira ya usambamba
mapatikana katika maelezo ya rana na anasa za masikani ya mamwinyi
yalinganishwapo na maelezo ya umaskim na unyonge wa masikani ya watu wa hali za
chini kama vile nyumbani kwa Mzee Sharwani.
Kwa upande wa ushairi pia, taswira za usambamba zimetumiwa na
washairi tofauti. Tutatoa mifano nuwili ya mashairi yaliyotumia taswira za namna
hii katika Matenga wa Bara. Mashairi hayo ni ya "Sima na Mayai" na
"Habari Mpya."
Katika shairi la "Sima na Mayai," maelezo ya maisha ya mkulima
masikini (beti za 2, 4, 6, 8, 10, 12, 13, 14, 15, 16, 17) yameelezwa, sambamba
na yale ya msomi mwenye nafasi nzuri kiuchumi (beti za 1, 3, 5, 7, 9 na 11).
Usambamba huu unatusaidia katika kulinganisha maisha ya watu wa aina hizo mbili.
Kutokana na taswira hizi za mlinganisho sisi wasomaji tunaiona
sima ya mtama upande nunoja, na upande wa pili tunaliona rundo la mayai si kwa
maana ya moja kwa moja ya vyakula hivyo, bali kwa dhana iletwayo na mlinganishao
wa taswira hizi mbili. Katika mlinganisho huu tunapata ufafanuzi wa ndani zaidi
unaohusu masuala ya elimu, siasa, uchumi, utaroaduni na utabaka wa jamii.
Taswira za usambamba na za mlinganisho zinajitokeza pia katika
shairi la "Habari Mpya". Humu tunalinganisha maneno ya Kasisi na ya "kijana
mmoja pandikizi", na hatimaye Kasisi anapofariki, tunaupata ujumbe uliokusudiwa.
Majigambo
Matumizi ya majigambo si jambo geni katika ushairi wa Kiswahili.
Tangu zamani yamekuwa yakitumika sana, hasa katika mashairi ya malumbano ambamo
washairi walijitapa na kuringia ushairi wao kwa nia ya kuwadunisha washairi
wengine walio "adui" zao katika mijadala mbalimbali.
Katika Malenga wa Bara mbinu hii ya majigambo haikutumiwa
sana, na pale ilipotumiwa imeongeza nguvu za shairi linalohusika. Katika shairi
la "Kauli ya Ununa" (uk.89) kwa mfano, washairi wameonyesha nguvu za kauli ya
umma kwa majigambo yaliyojengwa ndani ya tamathali ya sitiari. Umma umeitwa
"Nyundo" ambayo ina:
ulimi: ncha yenye kingo
Hukatisha nyemi, hubomoa nyongo
Ni mkoma wami ningiapo zogo.
Huu ni umma ulioshikamana kwa umoja kukataa ulwana.
Majigambo yamerudiwa katika shairi la "Soga" (uk.85) ambamo kwa
njiaya ucheshi washairi wanapinga "Unyama" (bila hasa kutueleza ni unyama gani
wanaouongelea) kwa kusema:
13. Jina langu Nyundo unanijua,
Kila nikidunda ninapasua...
14. Bali fuadini sitaki unyama!
Mtindo wa Tambo
Mtindo wa tambo hutumia mafumbo katika utoaji wa maudhui ya
shairi. Tambo huwa sawa na kitendawili ambacho msomaji anatakiwa akifumbue.
Katika malumbano washairi wengi walitumia mashairi ya tambu kuwafumbia washairi
wenzao ili wakune vichwa kwanza kabla ya kuvumbua yale yaliyokusudiwa na
waliyoaandika. Tumeona jinsi shairi ia "Vuteni Makasia" lilivyo tambo ambalo
ndani yake mmejificha maana ya uhuru.
Shairi la "Usemi wa Nyoka" nalo ni la tambo. Limetumia ucheshi
kwa kumtumia nyoka ambaye baada ya kujigamba mbele ya kadamnasi inambidi atoroke
harakaharaka ili kujihami na ghadhabu za tembo. Katika fumbo hili liko fundisho
kuwa kujitapa si tabia njema.
Shairi la "Asali na Nyuki" (uk. 83) nalo pia ni mfano mzuri wa
aina ya tambo; na katika fumbo hili msomaji anaweza kutoa maana mbalimbali.
Malhalani, asali huweza kuwa uhuru, mapenzi au jambo lolote lile analolitamani
mtu hadi anajitolea kwa hali na mali ili alipate.
Mtindo wa Vina na Mizani
Katika diwani ya Malenga wa Bara, washairi hawakufungwa
na mtindo wa aina moja wa ushairi. Humu imo mitindo mbalimbali, tangu ile ya
kimapokeo yenye mpangilio mahsusi wa vina, mizani, na beti, hadi ile ya kisasa
ambayo huamuliwa na kuainishwa na kile kiongelewacho. Kwa vile mtindo wa
kimapokeo umezoeleka kwa baadhi kubwa ya wasomaji, hatutaushughulikia humu.
Zaidi tutaangalia ile mitindo ambayo huenda ni migeni kwa wasomaji wengine
japokuwa watakapoichunguza kwa undani wanaweza kuigundua hata katika nyimbo na
ushairi wa makabila yao.
Katika shairi ia "Zuka" (uk. 7), washairi wameanza na ubeti
ufuatao kanuni za kimapokeo kwa kutupa mistari yenye nuzani minane minane ambayo
huishia na kina cha "ka". Ubeti wa pili wa shairi hili ni mchanganyiko wa
mitindo ambamo ndani yake kina cha "ma" kimctawala. Wamefanya makusudi kabisa
katika ukurasa uliotangulia kuandika katika mtindo wa mjazo uonekanao wa
kinathari. Mtindo huu umetumiwa kwa sababu kubwa mbili: Kwanza, kuonyesha
mabadiliko va msimuliaji kuwa sasa ni sauti ya watu na si ya msimuliaji wa nafsi
ya kwanza; na pili, kuonyesha kuwa dhana ya mistari katika beti za shairi ni
matokeo ya uandishi na kamwe isije kuchukulika kuwa kigezo cha sheria na kanuni
za ushairi wa Kiswahili.
Baada ya hapo, washairi wamebadili tena mtindo na kutupa ubeti
wenye kanuni sawa na ule wa kwanza. Kanuni hizi ni za mizani minane minane na
kina cha "ja" kwani maneno ya ubeti huu yanatolewa na sauti nyingine. Hata
katika ubeti unaofuatia yanatokea mabadiliko ya mtindo kwa sahabu hizo hizo.
Hapa kuna kina cha "ji" ambacho kinatokea ndani kwa ndani badala ya kuwekwa
katika sehemu mahsusi tu. ''Ubeti" wa mwisho, mfupi kuliko zote, ni wa
hitimisho ambalo linabeba uzito wa aina yake:
Watu wanasikia,
Tangazo la zinduko jipya,
Mimi nimeshasiksa.
Ni wazi kuwa "tangazo hili" linaonyesha uzalendo uliopevuka
zaidi ya ule wa kuipenda tu nchi tuukutao katika diwani ya kwanza ya washairi
hawa ya Mashairi ya Kisasa.
Kuhusu vina, wakati mwingine washairi hawa wameviweka vina
mwanzoni mwa baadhi ya mistari. Kwa mfano, katika shairi la "Jua la Dhahabu"
ubeti wa tatu neno "Waka" limeleta vina na mapigo ya aina yake katika mianzo ya
mistari kadhaa.
Washairi wanatumia sana mtindo wa marudiorudio ya maneno ili
kusisitiza jambo, na wakati huohuo kuleta mapigo ya aina fulani. Kwa mfano
katika mashairi ya "Siku Itafika" na "Siku Imefika" meneno ya vichwa hivyo
yamerudiwarudiwa sana kusisitiza kwanza tumaini jema la wanyonge, na pili
cherekochereko za ushindi. Vivyohivyo katika shairi la "Vilio vya Dhiki" jina la
shairi limerudiwarudiwa kuonyesha wingi wa vilio hivyohivyo vinavyodai haki.
Katika shairi la "Sima na Mayai", japokuwa kuna kumdiwarudiwa
kwa maneno "nikumbuke" na "kumbuka" ili kuwasisitizia vijana wasomi juu ya
umuhimu wa kuikumbuka na kuitumikia jamii iliyowasomesha, mtindo hasa uliotumika
ni ule wa ushairi huria wenye kulandana na msimuliaji (narrator) ambaye
ni mkulima mzee na masikini.
Hii ni mifano tu ya baadhi ya mitindo waliyoitumia washairi
hawa. Ni dhahiri kuwa iko mitindo mingi sana humu. Kwa mfano, japokuwa katika
shairi la "Mlima wa Kimombo" mtindo wa vina na mizani wa kimapokeo unatumika,
washairi wamechanganya pia mitindo mingine kufuatana na mambo tofautitofauti
wanayoyashughulikia.
Mara nyingi wasimuliaji katika mashairi haya ni wa nafsi ya
kwanza, "mimi", nafsi ambayo inafaulu kutufanya tuyaamini zaidi yale yasemwayo
kuwa yanatokana na uzoefu wa kuyaishi maisha wayaelezayo.
Labda kwa kumalizia tungetahadharisha tu kuwa Kahigi na Mulikozi
hawana vita wala uadui na ushain wa kimapokeo. Kwa hakika tukichunguza sana
zaidi ya nusu ya mashairi yao katika Malenga wa Bara ni ya kimapokeo
yenye kuzirigatia masuala ya vina na mizani. Jambo hili ameshindwa kuliona
Jumanne Mayoka ambaye upinzani wake katika kitabu chake cha Mgogoro wa
Ushairi na Diwani ya Mayoka (TPH, 1986) unaonyesha dhahiri kuwa hajakisoma
kitabu cha Malenga wa Bara. Tena wakati mwingine katika kujaribu
kuzingatia mno vipengele hivi vya vina na mizani baadhi ya mashairi ya Kahigi na
Mulokozi yamekuwa na udhaifu. Kwa mfano katika shairi la "Kwa Shaaban Robert"
ili kuleta mlingano wa kina cha "ni" kwenye beti za 3, 8, na 9, washairi
wametumia maneno "uliyoyaandikeni", "uliyotu-achieni" na "tunakuoneni", ambayo
husemwa kwa watu wengi na si kwa mtu mmoja kama walivyofanya hapa.
Udhaifu mwingine ni ule wa kawaida wa ngonjera za Mnyampala
ambamo mhusika mmoja hubadilika ghafla katika msimamo wake. Katika "Ngonjera"
(uk.43-49), ni vigumu kuamini mabadiliko ya mawazo ya Kijana anayeamka ghafla na
kuwa mwanamapinduzi wakati ambapo muda mfupi sana uliopita alikuwa mbumbumbu
hasa.
Hata hivyo, ni dhahiri kwamba Kahigi na Mulokozi wamefaulu
katika kushughulikia masuala mbalimbali ya kijamii-ya siasa, utamaduni na uchumi
- katika mashairi yao kwa kutumia ufundi wao wa t'ani katika kuyatolea maudhui
ya Malenga wo Bara.
Maswali
1. "Kahigi na Mulokozi wamefaulu kushughulikia masuala
mbalimbali ya kijamii na pia katika ufundl wao wa kisanii kwenye Malenga wa
Bara "Jadili.
2. "Kahigi na Mulokozi wanashauri katika baadhi kubwa ya
mashairi yao kwamba watu washike marungu, mapanga, bunduki na risasi wauane bila
sababu za kuridhisha." Jadili hoja hii na uthibitishe kwa mifano dhahiri.
3. Je, mawazo ya Kahigi na Mulokozi kuhusu Mungu, dini na maana
ya maisha ni yapi katika Malenga wa Bara? Unayaonaje mawazo hayo?
4. Chagua dhamira mbili kati ya zifuatazo na ujadili
zilivyojitokeza katika diwani ya Malenga wa Bara:
(a) Maanayauhuru
(b) Kumtetea mkulima
(c) Uzalendo
(d) Mapenzi.
5. Jadili kufaulu au kutokufaulu kwa fani ya mashairi ya
Malenga wa Bara katika kuyashughulikia maudhui.
6. Chagua vipengele vitatu vya fani ya ushairi kati ya
vifuatavyo na ujadili vilivyotumika katika Malenga wa Bara:
(a) Majigambo
(b) Misemo, methali na nahau
(c) Taswira ya safari
(d) Ishara
(e) Tamathali za semi.
Subscribe to:
Posts (Atom)